< Matthew 8 >
1 And when He came down from the mountain, great multitudes followed Him,
Wakati Yesu aliposhuka chini kutoka mlimani, umati mkubwa ulimfuata.
2 and behold, a leper having come, was prostrating to Him, saying, “Lord, if You are willing, You are able to cleanse me”;
Tazama, mkoma alikuja na kusujudu mbele yake, akasema, “Bwana, ikiwa uko tayari, unaweza kunifanya niwe safi”.
3 and having stretched forth the hand, Jesus touched him, saying, “I will, be cleansed,” and immediately his leprosy was cleansed.
Yesu akanyoosha mkono wake na kumgusa, akasema, “Niko tayari. Uwe msafi.” Hapo hapo alitakaswa ukoma wake.
4 And Jesus says to him, “See, you may tell no one, but go, show yourself to the priest, and bring the gift that Moses commanded for a testimony to them.”
Yesu akamwambia, “Angalia kwamba usiseme kwa mtu yeyote. Shika njia yako, na jioneshe mwenyewe kwa kuhani na utoe zawadi ambayo Musa aliagiza, kwa ajili ya ushuhuda kwao”
5 And Jesus having entered into Capernaum, there came to Him a centurion calling on Him,
Wakati Yesu alipofika Kapernaumu, Jemedari akaja kwake akamuuliza
6 and saying, “Lord, my young man has been laid in the house a paralytic, fearfully afflicted,”
akisema, “Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani amepooza na ana maumivu ya kutisha.”
7 and Jesus says to him, “I, having come, will heal him.”
Yesu akamwambia, “Nitakuja na kumponya”.
8 And the centurion answering said, “Lord, I am not worthy that You may enter under my roof, but only say a word, and my servant will be healed;
Jemedari akajibu na kumwambia, “Bwana, mimi si wathamani hata uje na kuingia ndani ya dari yangu, sema neno tu na mtumishi wangu ataponywa.
9 for I also am a man under authority, having under myself soldiers, and I say to this one, Go, and he goes, and to another, Be coming, and he comes, and to my servant, Do this, and he does [it].”
Kwa kuwa mimi pia ni mtu niliye na mamlaka, na ninao askari walio chini yangu. Nikisema kwa huyu “Nenda' na huenda, na kwa mwingine 'Njoo' na yeye huja, na kwa mtumishi wangu, 'Fanya hivi,' na yeye anafanya hivyo”
10 And Jesus having heard, wondered, and said to those following, “Truly I say to you, not even in Israel have I found such great faith;
Wakati Yesu aliposikia haya, alishangazwa na kuwaambia wale waliokuwa wakimfuata, “Kweli ninawaambia, Sijapata kuona mtu mwenye imani kama huyu katika Israel.
11 and I say to you that many from east and west will come and recline with Abraham, and Isaac, and Jacob, in the kingdom of the heavens,
Ninawambieni, wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, wataketi katika meza pamoja na Abrahimu, Isaka, na Yakobo, katika ufame wa mbinguni.
12 but the sons of the kingdom will be cast forth into the outer darkness—there will be the weeping and the gnashing of the teeth.”
Lakini watoto wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ambapo kutakuwa na kilio na kusaga meno.”
13 And Jesus said to the centurion, “Go, and as you believed let it be to you”; and his young man was healed in that hour.
Yesu akamwambia Jemadari, “Nenda! Kama ulivyokwisha amini, na itendeke hivyo kwako”. Na mtumishi aliponywa katika saa hiyo.
14 And Jesus having come into the house of Peter, saw his mother-in-law laid, and fevered,
Wakati Yesu alipofika kwenye nyumba ya Petro, alimwona mama mkwe wake na Petro amelala akiwa mgonjwa wa homa.
15 and He touched her hand, and the fever left her, and she arose, and was ministering to them.
Yesu akamgusa mkono wake, na homa yake ikamwacha. kisha akaamka akaanza kumhudumia.
16 And evening having come, they brought to Him many demoniacs, and He cast out the spirits with a word, and healed all who were ill,
Na ilipofika jioni, watu wakamletea Yesu wengi waliotawaliwa na pepo. Akawafukuza pepo na wale walio wagonjwa akawaponya.
17 that it might be fulfilled that was spoken through Isaiah the prophet, saying, “He took our sicknesses Himself, and bore the diseases.”
Kwa jinsi hii yalitimia yale yaliyo kwisha kunenwa na Isaya nabii, “Yeye mwenyewe alichukua magonjwa yetu na alibeba maradhi yetu”
18 And Jesus having seen great multitudes around Him, commanded to depart to the other side;
Kisha Yesu alipoliona kusanyiko limemzunguka, alitoa maelekezo ya kwenda upande mwingine wa Bahari ya Galilaya.
19 and a certain scribe having come, said to Him, “Teacher, I will follow You wherever You may go”;
Kisha mwandishi akaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, nitakufuata popote utakapoenda.”
20 and Jesus says to him, “The foxes have holes, and the birds of the sky places of rest, but the Son of Man has nowhere He may lay the head.”
Yesu akamwambia, “Mbweha wana mashimo, na ndege wa angani wana viota, lakini mwana wa Adamu hana sehemu ya kulaza kichwa chake.”
21 And another of His disciples said to Him, “Lord, permit me first to depart and to bury my father”;
Mwanafunzi mwingine akamwambia, “Bwana, niruhusu kwanza niende kumzika baba yangu.”
22 and Jesus said to him, “Follow Me, and permit the dead to bury their own dead.”
Lakini Yesu akamwambia, “Nifuate, na uwaache wafu wazike wafu wao.”
23 And when He entered into the boat His disciples followed Him,
Yesu alipoingia kwenye mtumbwi, wanafunzi wake wakamfuata mtumbwini.
24 and behold, a great storm arose in the sea, so that the boat was being covered by the waves, but He was sleeping,
Tazama, ikainuka dhoruba kuu juu ya bahari, kiasi kwamba mtumbwi ulifunikwa na mawimbi. Lakini Yesu alikuwa amelala.
25 and His disciples having come to Him, awoke Him, saying, “Lord, save us! We are perishing!”
Wanafunzi wakaja kwake na kumwamsha wakisema, “Bwana, tuokoe sisi, tunaelekea kufa!”
26 And He says to them, “Why are you fearful, O you of little faith?” Then having risen, He rebuked the winds and the sea, and there was a great calm;
Yesu akawaambia, “kwa nini mnaogopa, ninyi wenye imani ndogo?” Ndipo akaamka na kuukemea upepo na bahari. Kisha kukawa na utulivu mkuu,
27 and the men wondered, saying, “What kind—is this, that even the wind and the sea obey Him?”
wanaume wakashikwa na mshangao wakasema, “Huyu mtu niwa namna gani, kwamba hata pepo na bahari vinamtii yeye?”
28 And He having come to the other side, to the region of the Gergesenes, there met Him two demoniacs, coming forth out of the tombs, very fierce, so that no one was able to pass over by that way,
Wakati Yesu alipokuwa amekuja upande mwingine wa nchi ya Magadala, wanaume wawili waliotawaliwa na pepo walikutana naye. Walikuwa wakitokea makaburini na walikuwa wakifanya vurugu sana, kiasi kwamba hakuna msafiri angeweza kupita njia ile.
29 and behold, they cried out, saying, “What [regards] us and You, [[Jesus, ]] Son of God? Did You come here to afflict us before the time?”
Tazama, walipaza sauti na kusema, “Tuna nini cha kufanya kwako, mwana wa Mungu? Umekuja hapa kututesa kabla ya wakati kufika?”
30 And there was a herd of many pigs feeding far off from them,
Sasa kundi kubwa la nguruwe lilikuwa likichunga, hapakuwa mbali sana walipokuwa,
31 and the demons were calling on Him, saying, “If You cast us forth, permit us to go away into the herd of the pigs”;
pepo waliendelea kulalamika kwa Yesu na kusema. “Ikiwa utatuamuru kutoka, tupeleke kwenye kundi la nguruwe.”
32 and He says to them, “Go.” And having come forth, they went into the herd of the pigs, and behold, the whole herd of the pigs rushed down the steep, into the sea, and died in the waters,
Yesu akawaambia, “Nendeni!” Pepo wakawatoka na kwenda kwa nguruwe. Na tazama, kundi lote likashuka kutoka mlimani kuteremkia baharini na lote likafia majini.
33 and those feeding fled, and having gone into the city, they declared all, and the matter of the demoniacs.
Wanaume waliokuwa wakichunga nguruwe walikimbia. Na walipoenda mjini wakaelezea kila kitu, hususani kilichotokea kwa wanaume waliotawaliwa na mapepo.
34 And behold, all the city came forth to meet Jesus, and having seen Him, they called on [Him] that He might depart from their borders.
Tazama, mji mzima ukaja kukutana na Yesu. Walipomwona, walimsihi aondoke kwenye mkoa wao.