< Psalms 72 >

1 For Solomon. O God, give your judgment to the king, and your righteousness to the king's son;
Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
2 [that he may] judge your people with righteousness, and your poor with judgment.
Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
3 Let the mountains and the hills raise peace to your people:
Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
4 he shall judge the poor of the people in righteousness, and save the children of the needy; and shall bring low the false accuser.
Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
5 And he shall continue as long as the sun, and before the moon for ever.
Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
6 He shall come down as rain upon a fleece; and as drops falling upon the earth.
Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
7 In his days shall righteousness spring up; and abundance of peace till the moon be removed.
Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
8 And he shall have dominion from sea to sea, and from the river to the ends of the earth.
Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
9 The Ethiopians shall fall down before him; and his enemies shall lick the dust.
Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
10 The kings of Tharsis, and the isles, shall bring presents: the kings of the Arabians and Saba shall offer gifts.
Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
11 And all kings shall worship him; all the Gentiles shall serve him.
Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
12 For he has delivered the poor from the oppressor; and the needy who had no helper.
Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
13 He shall spare the poor and needy, and shall deliver the souls of the needy.
Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
14 He shall redeem their souls from usury and injustice: and their name [shall be] precious before him.
Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
15 And he shall live, and there shall be given him of the gold of Arabia: and [men] shall pray for him continually; [and] all the day shall they praise him.
Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
16 There shall be an establishment on the earth on the tops of the mountains: the fruit thereof shall be exalted above Libanus, and they of the city shall flourish as grass of the earth.
Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
17 Let his name be blessed for ever: his name shall endure longer than the sun: and all the tribes of the earth shall be blessed in him: all nations shall call him blessed.
Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
18 Blessed is the Lord God of Israel, who alone does wonders.
Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
19 And blessed is his glorious name for ever, even for ever and ever: and all the earth shall be filled with his glory. So be it, so be it.
Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
20 The hymns of David the son of Jessae are ended.
Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu

< Psalms 72 >