< Proverbs 26 >
1 As snow in summer, and as rain in harvest, so honour is not suitable for a fool.
Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
2 As the bird by wandering, as the swallow by flying, so the curse causeless shall not come.
Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
3 A whip for the horse, a bridle for the ass, and a rod for the fool's back.
Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
4 Answer not a fool according to his folly, lest you also be like unto him.
Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
5 Answer a fool according to his folly, lest he be wise in his own conceit.
Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
6 He that sends a message by the hand of a fool cuts off the feet, and drinks damage.
Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
7 The legs of the lame are not equal: so is a parable in the mouth of fools.
Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
8 As he that binds a stone in a sling, so is he that gives honour to a fool.
Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
9 As a thorn goes up into the hand of a drunkard, so is a parable in the mouths of fools.
Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
10 The great God that formed all things both rewards the fool, and rewards transgressors.
Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
11 As a dog returns to his vomit, so a fool returns to his folly.
Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
12 See you a man wise in his own conceit? there is more hope of a fool than of him.
Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
13 The slothful man says, There is a lion in the way; a lion is in the streets.
Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
14 As the door turns upon his hinges, so does the slothful upon his bed.
Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
15 The slothful hides his hand in his bosom; it grieves him to bring it again to his mouth.
Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
16 The sluggard is wiser in his own conceit than seven men that can render a reason.
Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
17 He that passes by, and meddles with strife belonging not to him, is like one that takes a dog by the ears.
Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
18 As a mad man who casts firebrands, arrows, and death,
Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
19 So is the man that deceives his neighbour, and says, Am not I in sport?
ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
20 Where no wood is, there the fire goes out: so where there is no talebearer, the strife ceases.
Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
21 As coals are to burning coals, and wood to fire; so is a contentious man to kindle strife.
Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
22 The words of a talebearer are as wounds, and they go down into the innermost parts of the belly.
Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
23 Burning lips and a wicked heart are like a potsherd covered with silver dross.
Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
24 He that hates dissembles with his lips, and lays up deceit within him;
Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
25 When he speaks fair, believe him not: for there are seven abominations in his heart.
Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
26 Whose hatred is covered by deceit, his wickedness shall be showed before the whole congregation.
Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
27 Whoso digs a pit shall fall therein: and he that rolls a stone, it will return upon him.
Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
28 A lying tongue hates those that are afflicted by it; and a flattering mouth works ruin.
Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.