< Romans 5 >

1 BEING justified therefore by faith, we have peace with God through our Lord Jesus Christ:
Kwa kuwa tumehesabiwa haki kwa njia ya imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
2 by whom also we have had an introduction through faith into this grace in which we have stood fast, and are rejoicing in hope of the glory of God.
Kupitia yeye sisi pia tuna fursa kwa njia ya imani katika neema hii ambayo ndani yake tunasimama. Tunafurahi katika ujasiri atupao Mungu kwa ajili ya baadaye, ujasiri ambao tutashiriki katika utukufu wa Mungu.
3 And not only so, but we glory also in tribulations: knowing that tribulation produceth patience;
Siyo hili tu, lakini pia tunafurahi katika mateso yetu. Tunajua kwamba mateso huzaa uvumilivu.
4 and patience, proof; and proof, hope;
Uvumilivu huzaa kukubalika, na kukubalika huzaa ujasiri kwa ajili ya baadaye.
5 and hope doth not make us ashamed; because the love of God is poured out into our hearts by the Holy Ghost which is given to us.
Ujasiri huu haukatishi tamaa, kwa sababu upendo wa Mungu umemwagwa katika mioyo yetu kupitia Roho Mtakatifu, ambaye alitolewa kwetu.
6 For even then when we were without strength, Christ died in due time for the ungodly.
Kwa tulipokuwa tungali tu dhaifu, kwa wakati muafaka Kristo alikufa kwa ajili ya waovu.
7 For scarcely for a righteous person will any one die: though for a good man perhaps some one might even dare to die.
Kwa kuwa itakuwa vigumu mmoja kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki. Hii ni kwamba, pengine mtu angethubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
8 But God commendeth his own love towards us, that, though we were yet sinners, Christ died in our stead.
Lakini Mungu amehakikisha upendo wake mwenyewe kwetu, kwa sababu wakati tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
9 Therefore much more, being justified already by his blood, shall we be saved by him from wrath.
Kisha zaidi ya yote, sasa kwa kuwa tumehesabiwa haki kwa damu yake, tutaokolewa kwa hiyo kutoka katika gadhabu ya Mungu.
10 For if, being enemies, we have been reconciled to God by the death of his son, much more, having been reconciled, shall we be saved by his life.
Kwa kuwa, ikiwa wakati tulipokuwa maadui, tulipatanishwa na Mungu kwa njia ya kifo cha mwanae, zaidi sana, baada ya kuwa tumekwisha patanishwa, tutaokolewa kwa maisha yake.
11 And not so only, but we exult in God through our Lord Jesus Christ, through whom already we have received reconciliation.
Siyo hivi tu, bali pia tunafurahi katika Mungu kupitia Bwana Yesu Kristo, kupitia yeye ambaye sasa tumepokea upatanisho huu.
12 Therefore, as by one man sin entered into the world, and by sin death; even so death passed into all men through him, in whom all have sinned.
Kwa hiyo basi, kama kupitia mtu mmoja dhambi iliingia duniani, kwa njia hii kifo kiliingia kwa njia ya dhambi. Na kifo kikasambaa kwa watu wote, kwa sababu wote walifanya dhambi.
13 For until the law sin was in the world: but sin is not imputed if there be no law.
Kwa kuwa hadi sheria, dhambi ilikuwa duniani, lakini dhambi haihesabiki wakati hakuna sheria.
14 But death reigned from Adam unto Moses, even over those who have not sinned after the similitude of the transgression of Adam, who is a type of him that was to come.
Hata hivyo, kifo kilitawala kutoka Adamu hadi Musa, hata juu ya wale ambao hawakufanya dhambi kama kutotii kwa Adamu, ambaye ni mfano wa yeye ambaye angekuja.
15 But not as the transgression, so also is the gift. For if by the transgression of one the many became dead, much more the grace of God, and the gift by grace, which is in that one man, Christ Jesus, hath abounded unto many.
Lakini hata hivyo, zawadi ya bure si kama kosa. Kwa kuwa ikiwa kwa kosa la mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu na zawadi kwa neema ya mtu mmoja, Yesu Kristo, imezidi kuongezeka kwa wengi.
16 And the gift is not as for one who sinned: for the judgment indeed came by one to condemnation, but the free gift leads to justification from many offences.
Kwa kuwa zawadi si kama matokeo ya yule ambaye alifanya dhambi. Kwa kuwa kwa upande mwingine, hukumu ya adhabu ilikuja kwa sababu ya kosa la mtu mmoja. Lakini kwa upande mwingine, kipawa cha bure kinachotoka katika kuhesabiwa haki kilikuja baada ya makosa mengi.
17 For if by the offence of one, death reigned by that one; much more they who receive the abundance of grace, and of the gift of righteousness, shall reign in life by one, Christ Jesus.
Kwa maana, ikiwa kwa kosa la mmoja, kifo kilitawala kupitia mmoja, zaidi sana wale ambao watapokea neema nyingi pamoja na kipawa cha haki watatawala kupitia maisha ya mmoja, Yesu Kristo.
18 Well then, as by the offence of one, judgment issued against all men unto condemnation; so also by the righteousness of one, the gift came to all men for justification unto life.
Hivyo basi, kama kupitia kosa moja watu wote walikuja kwenye hukumu, ingawa kupitia tendo moja la haki kulikuja kuhesabiwa haki ya maisha kwa watu wote.
19 For as by the disobedience of one man the many were constituted sinners; so also by the obedience of one shall the many be constituted righteous.
Kwa kuwa kama kupitia kutotii kwa mtu mmoja wengi walifanywa wenye dhambi, hivyo kupitia utii wa mmoja wengi watafanywa wenye haki.
20 But the law was introduced, that the offence might be more abundant. But where sin had abounded, there hath grace abounded more exceedingly:
Lakini sheria iliingia pamoja, ili kwamba kosa liweze kuenea. Lakini mahali ambapo dhambi ilizidi kuwa nyingi, neema iliongezeka hata zaidi.
21 that as sin had reigned by death, even so might grace reign through righteousness unto life eternal by Jesus Christ our Lord. (aiōnios g166)
Hii ilitokea ili kwamba, kama dhambi ilivyotawala katika kifo, ndivyo hata neema inaweza kutawala kupitia haki kwa ajili ya maisha ya milele kupitia Yesu Kristo Bwana wetu. (aiōnios g166)

< Romans 5 >