< Romans 12 >

1 I BESEECH you, therefore, brethren, by the mercies of God, to present your bodies a living sacrifice, holy, acceptable to God, which is your reasonable service.
Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
2 And be not conformed to this world, but be transformed by the renovation of your mind, that you may prove by experience what is the will of God, that is good, acceptable, and perfect. (aiōn g165)
Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
3 For, I say, by the grace which is given unto me, to every one that is among you, not to think of himself above what he ought to think; but to think soberly, as God has divided to every one the measure of faith.
Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
4 For as we have in one body many members, but the members, though many, have not the same function,
Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
5 so we, being many, are one body in Christ, and every one reciprocally members of each other.
Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
6 Having then different gifts according to the grace which is given unto us, if it be prophecy, speak according to the analogy of faith;
Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
7 or if the deacon’s office, be active in the service; or he that teacheth, in teaching;
Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
8 or he that exhorteth, in exhortation; he that distributes, let him do it with simplicity; he that presideth, with diligence; he that is employed in acts of mercy, with cheerfulness.
Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
9 Let love be undissembled. Abhor that which is evil; cleave to that which is good.
Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
10 In brotherly affection be tenderly attached to each other; in honour preferring one another:
Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
11 not slothful in business; fervent in spirit; serving the Lord:
Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
12 rejoicing in hope; patient in affliction; persevering in prayer:
Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
13 communicating to the wants of the saints; prompt to hospitality.
Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
14 Bless them who persecute you; bless, and curse not.
Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
15 Rejoice with those that rejoice, and weep with those that weep.
Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
16 Be of the same mind among each other. Affect not high things, but be condescending to the lowly. Be not wise in your own conceits.
Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
17 Render to no man evil for evil. Be provident of things laudable in the sight of all men.
Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
18 If possible, as far as you can, be at peace with all men.
Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
19 Avenge not yourselves, beloved, but give place unto wrath: for it is written, “Vengeance belongeth to me; I will recompence, saith the Lord.”
Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
20 If therefore thine enemy hunger, give him food; if he thirst, give him drink: for so doing, thou shalt heap up coals of fire on his head.
“Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
21 Be not overcome of evil, but overcome evil with good.
Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.

< Romans 12 >