< Matthew 7 >

1 JUDGE not, that ye be not judged.
Usihukumu, nawe usije ukahukumiwa.
2 For with the same judgment ye judge others, shall ye be judged: and with the measure ye mete, shall it be measured to you again.
Kwa hukumu unayohukumu, nawe utahukumiwa. Na kwa kipimo unachopima na wewe pia utapimiwa hicho hicho.
3 And why spiest thou out the mote which is in thy brother’s eye, yet payest no attention to the beam which is in thine own eye?
Na kwa nini unatazama kipande cha mti kilichoko kwenye jicho la ndugu yako, lakini hutambuwi kipande cha gogo ambalo limo katika jicho lako?
4 Or how wilt thou say to thy brother, Suffer me to take the mote off from thine eye: and behold there is a beam in thine own eye?
Unawezaje kusema kwa ndugu yako, ngoja nikutolee kipande kilichomo kwenye jicho lako, wakati kipande cha gogo kimo ndani ya jicho lako?
5 Thou hypocrite, take first the beam out of thine own eye and then shalt thou see clearly to take off the mote from thy brother’s eye.
Mnafiki wewe; kwanza toa gogo lililomo kwenye jicho lako, na ndipo utakapoweza kuona vizuri na kukitoa kipande cha mti kilichomo kwenye jicho la ndugu yako.
6 Give not that which is holy to dogs, nor cast pearls before swine; lest they tread them under foot, and turning round tear you.
Usiwape mbwa kilicho kitakatifu, na usiwarushie nguruwe lulu mbele yao. Vinginevyo wataviharibu na kuvikanyaga kwa miguu, na tena watakugeukia wewe na kukurarua vipande vipande.
7 Ask, and it shall be given you; seek, and ye shall find; knock, and it shall be opened unto you:
Omba, nawe utapewa. Tafuta, nawe utapata. Bisha hodi, na wewe utafunguliwa.
8 for every one that asketh receiveth; and he that seeketh findeth; and to him that knocketh it shall be opened.
Kwa yeyote anayeomba, hupokea. Na kwa yeyote anayetafuta, hupata. Na kwa mtu ambaye anayebisha hodi, atafunguliwa.
9 What man is there of you, of whom if his son ask a loaf, will he give him a stone?
Au kuna mtu miongoni mwenu ambaye, ikiwa mtoto wake amemwomba kipande cha mkate atampa jiwe?
10 or if he ask a fish, will he give him a serpent?
Au ikiwa atamwomba samaki, na yeye atampa nyoka?
11 If ye then, evil as ye are, know how to bestow good gifts on your children; how much more will your Father who is in heaven, bestow good things on those who ask him?
Kwa hiyo, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, Je! Ni kiasi gani zaidi Baba aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wanao muomba yeye?
12 All things therefore whatsoever ye would be willing that men should do to you, just so do ye to them: for this is the law and the prophets.
Kwa sababu hiyo, unapotaka kufanyiwa kitu chochote na watu wengine, nawe pia itakupasa kuwafanyia hivyo hivyo wao. Kwa kuwa hiyo ni sheria na manabii.
13 Enter in through the strait gate: for wide is the gate, and spacious the road, which leadeth to perdition, and they are many who enter that way:
Ingieni kwa kupitia geti jembamba. Kwa kuwa geti ni pana na njia ni pana inayoongoza kwenye uharibifu, na kuna watu wengi wanaopitia njia hiyo.
14 because strait is the gate, and narrow the road, which leadeth to life, and they are but a few who find it.
Geti ni jembamba, Geti jembamba ni njia inayongooza katika uzima na ni wachache wanaoweza kuiona.
15 Take heed then of false prophets, who come to you in the garb of sheep, but inwardly they are ravening wolves.
Jihadhari na manabii wa uongo, wanaokuja wamevaa ngozi ya kondoo, lakini kweli ni mbweha wakali.
16 By their fruits ye shall know them. Do men gather a bunch of grapes from thorns, or figs from thistles?
Kwa matunda yao mtawatambua. Je watu wanaweza kuvuna matunda kwenye miba, au mtini kwenye mbengu ya mbaruti?
17 So every good tree beareth good fruits; but every bad tree in kind, produceth bad fruits.
Kwa jinsi hiyo, kila mti mzuri huzaa matunda mazuri, lakini mti mbaya huzaa matunda mabaya.
18 A good tree cannot produce bad fruits, neither can a tree bad in kind produce good fruits.
Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
19 Every tree that beareth not good fruit, is cut down, and cast into the fire.
Kila mti ambao hauzai matunda mazuri utakatwa na kutupwa katika moto.
20 Well then! by their fruits ye shall know them.
Hivyo basi, utawatambua kutokana na matunda yao.
21 Not every one who saith to me, Lord, Lord! shall enter into the kingdom of heaven; but he that doeth the will of my Father who is in heaven.
Si kila mtu aniambiaye mimi, 'Bwana, Bwana,' ataingia katika ufalme wa mbinguni, bali ni yule pekee atendaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Many will say unto me in that day, Lord, Lord, have we not prophesied in thy name? and in thy name have we not cast out devils? and in thy name done many miracles?
Watu wengi wataniambia siku hiyo, 'Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, hatukutoa mapepo kwa jina lako, na kwa jina lako tulifanya matendo mengi makuu?'
23 And then will I profess unto them, that I never knew you: depart from me, ye workers of iniquity.
Ndipo nitawaambia wazi, 'sikuwatambua ninyi! Ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu!'
24 Every man therefore who is hearing from me these words, and puts them in practice, I will compare him to the intelligent man, who erected his house upon a rock:
Kwa hiyo, kila mmoja asikiaye maneno yangu na kutii atafanana na mtu mwenye hekima aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.
25 and the rain descended, and the rivers rushed, and the winds blew, and they beat against that house, and it fell not; for it was founded on a rock.
Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukaja na ukaipiga nyumba hiyo, lakini haikuweza kuanguka chini, kwa kuwa ilikuwa imejengwa juu ya mwamba.
26 And every man who is hearing these sayings of mine, and doth not practise them, he will resemble the foolish man, who built his house upon the sand:
Lakini kila mtu anayesikia neno langu na asilitii, atafananishwa na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.
27 and the rain descended, and the rivers rushed, and the winds blew, and set against that house, and it fell; and the fall of it was great.
Mvua ikaja, mafuriko yakaja, na upepo ukaja na kuipiga nyumba hiyo. Na ikaanguka, na uharibifu wake ukakamilika.”
28 And it was so, that when Jesus had concluded all these sayings, the multitudes were exceedingly struck with his teaching:
Ulifika wakati ambao Yesu alipomaliza kuongea maneno haya, makutano walishangazwa na mafundisho yake,
29 for he taught them as having authority, and not as the scribes.
kwa kuwa alifundisha kama mtu mwenye mamlaka, na si kama waandishi wao.

< Matthew 7 >