< Matthew 14 >

1 AT that time Herod the tetrarch heard the report of Jesus,
Kwa wakati huo, Herode alisikia habari juu ya Yesu.
2 and said unto his servants, This is John the Baptist; he is risen from the dead, and therefore miracles are wrought by him.
Akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji amefufuka kutoka katika wafu. Kwa hiyo nguvu hizi zipo juu yake.”
3 For Herod having seized John, had bound him, and put him in prison, for the sake of Herodias, the wife of Philip his brother.
Kwa kuwa Herode alikuwa amemkamata Yohana akamfunga na kumtupa gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo kaka yake.
4 For John said unto him, It is unlawful for thee to have her.
Kwa kuwa Yohana alimwambia, “Si halali kumchukua yeye kuwa mke wake.”
5 And though he wished to kill him, he was afraid of the multitude, for they held him as a prophet.
Herode angemwua lakini aliwaogopa watu kwa sababu walimwona Yohana kuwa nabii.
6 But when Herod’s birth-day was kept, the daughter of Herodias danced in the circle, and pleased Herod:
Lakini wakati siku ya kuzaliwa Herode ilipofika binti wa Herodia alicheza katikati ya watu na kumpendeza Herode.
7 so that with an oath he promised to give her whatever she should ask.
Katika kujibu kili aliahidi kwa kiapo kwamba atampa chochote atakachoomba.
8 And she, being previously urged on by her mother, said, Give me here, in a spacious dish, the head of John the Baptist.
Baada ya kushauriwa na mama yake, alisema, “Nipe mimi hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
9 And the king was grieved: but for his oath’s sake, and on account of those who were with him, he commanded it to be given her.
Mfalme alikuwa na sikitiko kwa maombi ya binti, lakini kwa ajili ya kiapo chake, kwa sababu ya wote waliokuwa chakulani pamoja naye aliamuru kwamba inapaswa ifanyike.
10 And he sent, and beheaded John in the prison.
Alituma Yohana aletwe kutoka gerezani
11 And his head was brought on a large dish, and was given to the young lady: and she brought it to her mother.
ili akatwe kichwa chake na kikaletwa juu ya sinia na akapewa binti na akakipeleka kwa mama yake.
12 And his disciples came and took the body, and buried it, and they came and told Jesus.
Kisha wanafunzi wake wakaja kuuchukua ule mwili na kuuzika, baada ya hili walienda kumwambia Yesu.
13 And when Jesus heard it, he withdrew from thence in a vessel into a desert place apart: and when the multitudes heard it, they followed him on foot from the cities.
Naye Yesu aliposika haya, akijatenga kutoka mahali pale akapanda ndani ya mashuka akaenda sehemu iliyotengwa. Wakati umati ulipo fahamu alikokuwa, walimfuata kwa miguu kutoka mijini.
14 And when Jesus was come forth, he saw a great multitude, and was moved with compassion towards them, and healed their sick.
Kisha Yesu alikuja mbele yao akauona umati mkubwa. Akawaonea huruma na kuponya magonjwa yao.
15 But when evening was come, his disciples came unto him, saying, The place is desert, and the day is far advanced; send the multitude away, that they may go into the villages, and buy themselves provisions.
Jioni ilipotimia, wanafunzi wakaja kwake na kusema, “Hii ni sehemu ya jangwa, na siku tayari imepita. Watawanyishe makutano ili waende vijijini wakanunue chakula kwa ajili yao.
16 But Jesus said unto them, They need not depart: give ye them to eat.
Lakini Yesu akawaambia, ''Hawana haja ya kwenda zao. Wapeni ninyi chakula”
17 And they said unto him, We have nothing here except five loaves and two fishes.
Wakamwambia, ''Hapa tunayo mikate mitano na samaki wawili tu.”''
18 Then he said, Bring them hither to me.
Yesu akasema, “Ileteni kwangu.”
19 And he commanded the multitude to sit down on the grass, and taking the five loaves and the two fishes, looking up to heaven, he blessed them, and brake, and gave the loaves to the disciples, and the disciples to the multitude.
Kisha Yesu akauamuru umati kukaa chini ya nyasi. Akachukuwa mikate mitano na samaki wawili. Akatazama juu mbinguni, akabariki na kumega mikate akawapa wanafunzi. Wanafunzi wakaupatia umati.
20 And they did all eat, and were filled: and they took up the superabundance of the fragments, twelve baskets full.
Wakala wote na kushiba. Kisha wakavikusanya vipande vyote vya chakula na kujaza vikapu kumi na mbili.
21 And they who had eaten, were about five thousand men, besides women and children.
Wale waliokula walikadiriwa kuwa wanaume elfu tano bila ya kusehabu wanawake na watoto.
22 And immediately Jesus compelled his disciples to go on board the vessel, and pass before him to the other side, while he dismissed the people.
Mara moja aliwaamuru wanafunzi waingie ndani ya mashua, wakati huo yeye akawaaga umati waende zao.
23 And when he had sent away the multitude, he went up into a mountain apart to pray: and when evening came, he was there alone.
Baada ya kuwaaga umati kwenda zao, akapanda juu mlimani kuomba pekee yake. Wakati ilipokuwa jioni alikuwa huko pekee yake.
24 But the vessel was already in the midst of the sea, tossed with the waves: for the wind was contrary.
Lakini sasa mashua ilipokuwa katikati ya bahari ukiyumbayumba kwa sababu ya mawimbi, kwani upepo ulikuwa wa mpisho.
25 Then at the fourth watch of the night came Jesus unto them, walking on the sea.
Katika usiku wa zamu ya nne Yesu aliwakaribia, akitembea juu ya maji.
26 And when the disciples saw him walking on the sea, they were greatly agitated, saying, It is his apparition. And they cried out with terror.
Wakati wanafunzi wake walipomwona akiitembea juu ya bahari, walihofu na kusema, “Ni mzuka,'' na kupaaza sauti katika hali ya uoga.
27 And immediately Jesus spake to them, saying, Be of good courage: it is I; be not terrified.
Yesu akawaambia mara moja, akisema, “Jipeni moyo! ni mimi! msiogope.”
28 Then Peter answering, said, Lord, if it be thou, command me to come unto thee upon the waters.
Petro alimjibu kwa kusema, “Bwana, kama ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.''
29 And he said, Come. And descending from the vessel, Peter walked upon the waters to come to Jesus.
Yesu akasema, “Njoo.'' Hivyo Petro akatoka ndani ya mashua na akatembea juu ya maji kwenda kwa Yesu.
30 But seeing the wind boisterous, he was afraid; and beginning to sink in the deep, he cried out, saying, Lord save me.
Lakini Petro alipoona mawimbi, aliogopa, na kuanza kuzama, chini, akaita sauti na kusema, “Bwana, niokoe!''
31 Then immediately Jesus stretching out his hand, laid hold on him, and said to him, O thou of little faith, wherefore dost thou doubt?
Haraka Yesu akanyoosha mkono wake akamnyanyua Petro, na kumwambia, “Wewe mwenye imani ndogo, kwa nini ulikuwa na mashaka?”
32 And when they came aboard the vessel, the wind ceased.
Ndipo Yesu na Petro walipoingia katika mashua, upepo ulikoma kuvuma.
33 And they who were in the vessel, came and worshipped him, saying, Truly thou art the Son of God.
Wanafunzi mashuani wakamwabudu Yesu na kusema, “Kweli wewe ni Mwana wa Mungu.”
34 And passing over, they came to the land of Gennesareth.
Na walipokwisha kuvuka, walifika katika nchi ya Genesareti.
35 And when the men of that place knew him, they sent into all that neighbourhood, and brought to him all that had illnesses:
Na watu katika eneo lile walipomtambua Yesu, walituma ujumbe kila sehemu za kando, na kuleta kila aliyekuwa mgonjwa.
36 and they besought him that they might only touch the fringe of his garment: and as many as touched it were cured.
Walimsihi kwamba waweze kugusha pindo la vazi lake, na wengi walioligusa waliponywa.

< Matthew 14 >