< Luke 1 >
1 SINCE many have attempted to compose a narrative of facts, confirmed to us by the fullest evidence:
Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
2 exactly as they delivered them to us, who were eve witnesses from the first, and ministers of the word;
kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
3 it seemed right to me also, having obtained accurate knowledge of all things from above, to write to thee in regular order, most excellent Theophilus,
Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
4 to the intent that thou mayest clearly know the certainty of those matters, concerning which thou hast been instructed.
Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
5 There was in the days of Herod, the king of Judea, a certain priest named Zacharias, of the course of Abiah: and his wife of the daughters of Aaron, and her name Elisabeth.
Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
6 And they were both righteous before God, walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
7 And they had no child, because Elizabeth was barren, and both were far advanced in years.
Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
8 And it came to pass, as he discharged his priestly office in the order of his periodical ministration before God,
Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
9 according to the custom of the priesthood, it fell to his lot to burn the incense when he went into the temple of the Lord.
Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
10 And all the multitude of people was praying without, at the time of the burning the incense.
Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
11 And an angel of the Lord appeared to him standing on the right side of the altar of incense.
Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
12 And Zacharias was agitated greatly at the sight, and fear fell upon him.
Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
13 But the angel said unto him, Fear not, Zacharias: for thy prayer is heard; and thy wife Elisabeth shall bring thee a son, and thou shalt call his name John.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
14 And it shall give thee joy and exultation; and many shall rejoice at his birth:
Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 for he shall be great in the sight of the Lord; and he shall never drink wine, nor any intoxicating liquor; and he shall be filled with the Holy Ghost, even from his mother’s womb.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 And many of the children of Israel shall he turn unto the Lord, their God.
Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
17 And he shall go forth before him in the spirit and power of Elias, to convert the hearts of fathers with their children, and the disobedient to the wisdom of the just; to prepare a people ready for the Lord.
Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
18 And Zacharias said to the angel, By what shall I know this? for I am old, and my wife far advanced in her age.
Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
19 And the angel answering said to him, I am Gabriel, that stand in the presence of God; and I have been sent to speak to thee, and to proclaim these glad tidings to thee.
Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
20 And behold, thou shalt be dumb, and unable to speak, until that day when these things shall come to pass, because thou hast not believed my words, which shall be fulfilled at their exact time.
Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
21 And the people were waiting for Zacharias, and marvelled that he tarried so long in the temple.
Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
22 And when he came out, he could not speak to them: and they perceived that he had seen a vision in the temple: for he himself made signs to them, and continued deaf and dumb.
Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
23 And it came to pass, when the days of his ministry were fulfilled, he went to his own house.
Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
24 And after those days Elisabeth his wife conceived, and kept herself in retirement five months, saying,
Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
25 Thus hath the Lord dealt with me in the days in which he looked upon me to take away my reproach among men.
“Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
26 Now in the sixth month the angel Gabriel was sent from God into a city of Galilee, the name of which was Nazareth,
Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
27 to a virgin of the house of David, betrothed to a man whose name was Joseph; and the virgin’s name was Mary.
kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
28 And the angel coming in to her said, All hail! O thou highly favoured one! the Lord is with thee: blessed art thou among women.
Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
29 And when she saw him, she was greatly agitated at his address: and reasoned in herself what kind of salutation this could be.
Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
30 And the angel said unto her, Fear not, Mary, for thou hast found favour with God.
Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
31 And, behold, thou shalt conceive in thy womb, and bring forth a son, and thou shalt call his name JESUS.
Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
32 He shall be great, and shall be called the Son of the Highest: and the Lord God will give him the throne of David his father;
Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 and he shall reign over the house of Jacob for ever, and of his kingdom there shall be no end. (aiōn )
Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn )
34 And Mary said, How shall this be, seeing I know not man?
Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
35 And the angel answering said unto her, The Holy Ghost shall come upon thee, and the power of the Most High shall overshadow thee; wherefore also the Holy One that shall be born of thee, shall be called the Son of God.
Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
36 And, behold, Elisabeth thy cousin, she also hath conceived in her old age: and this is the fifth month of pregnancy with her who was called barren.
Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
37 For there is nothing impossible with God.
Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
38 Then said Mary, Behold a servant of the Lord, be it to me according to thy declaration. And the angel departed from her.
Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
39 Then Mary arose in those days, and went with haste into the hill country, to a city of Judah,
Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
40 and entered into the house of Zachariah, and saluted Elisabeth.
Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
41 And it came to pass, when Elisabeth heard the salutation of Mary, the babe leaped for joy in her womb; and Elisabeth was filled with the Holy Ghost:
Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
42 and she exclaimed with a loud voice, and said, Blessed art thou among women, and blessed is the fruit of thy womb.
Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
43 And whence is this favour shewn me, that the mother of my Lord should come to me?
Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
44 For, lo! as the voice of thy salutation reached my ears, the babe leaped for joy in my womb.
Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
45 And blessed is she that hath believed; for there shall be a fulfilment of the things told her from the Lord.
Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
46 And Mary said, My soul doth magnify the Lord,
Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
47 and my spirit hath exulted in God my Saviour:
na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
48 for he hath looked upon the lowly state of his maid-servant: for, lo! henceforth shall all generations pronounce me blessed.
Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
49 For the Mighty One hath done great things for me; and holy is his name.
Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
50 And his mercy is upon those who fear him, from generation to generation.
Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
51 He hath displayed strength from his arm; he hath scattered the proud in the imagination of their hearts.
Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
52 He hath cast down potentates from the throne, and hath exalted the lowly.
Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
53 He hath filled the hungry with good things; and the rich he hath sent empty away.
Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 He hath succoured Israel his servant, that he might be mindful of mercy for ever; (aiōn )
Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
55 as he had spoken to our fathers, to Abraham, and to his seed.
(kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn )
56 And Mary abode with her about three months, and returned unto her home.
Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
57 Now Elisabeth’s time was up that she should be delivered; and she brought a son.
Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
58 And her neighbours and her relations heard, that the Lord had magnified his mercy upon her; and they congratulated her.
Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
59 And it came to pass, on the eighth day they came to circumcise the child; and they called him after the name of his father, Zacharias.
Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
60 And his mother spake and said, No; but he shall be called John.
Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
61 And they said to her, There is not one among thy relations, who is called by this name.
Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
62 And they made signs to his father, what he would have him called.
Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
63 And desiring a writing tablet, he wrote, saying, John is his name. And they were all surprised.
Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
64 Instantly then his mouth was opened, and his tongue loosed, and he burst out in praises to God.
Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
65 And great awe fell on all those who dwelt around them: and in all the mountainous country of Judea, all these circumstances were the subject of conversation.
Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
66 And all who heard them laid them up in their hearts, saying, Well! what a child will this be! And the hand of the Lord was with him.
Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 And Zacharias his father was filled with the Holy Ghost, and prophesied, saying,
Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
68 Blessed be the Lord the God of Israel; for he hath visited and wrought redemption for his people;
“Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
69 and hath raised up a horn of salvation for us in the house of his servant David:
Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
70 as he spake by the mouth of his holy prophets, which have been from the beginning: (aiōn )
kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn )
71 even preservation from our enemies, and from the hand of all that hate us;
Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 to perform mercy towards our fathers, and to remember his own holy covenant:
Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
73 the oath which he sware to Abraham our father,
kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
74 to give us, that we, secure from fear, rescued from the hands of our enemies, should serve him,
Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
75 in righteousness and holiness before him, all the days of our life.
katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
76 And thou, child, shalt be called the prophet of the Most High; for thou shalt go before the face of the Lord to prepare his ways;
Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
77 to give the knowledge of salvation to his people, by the remission of their sins,
kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
78 through the bowels of mercy of our God; with which he hath visited us, as the dawn of the morning from on high,
Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
79 to illumine those who sat in darkness, and in the shadow of death, to direct our feet into the way of peace.
kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
80 And the child grew, and became mighty in spirit, and was in the deserts until the days of his public exhibition to Israel.
Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.