< Acts 28 >
1 AND being safe landed, we then understood that the island was called Melita.
Tulipofikishwa salama, tulitambua kwamba kisiwa kinaitwa Malta.
2 And the rude people treated us with singular humanity; for, lighting a fire, they received us all, because of the violent rain, and because of the cold.
Watu wenyeji wa pale si tu kwamba walitupa ukarimu wa kawaida, bali waliwasha moto na kutukaribisha sote, kwa sababu ya mvua na baridi iliyokuwa ikiendelea.
3 But as Paul was gathering up a faggot of sticks, and laying them on the fire, there came a viper out of the heat, and fastened on his hand.
Lakini Paulo alipokuwa amekusanya mzigo wa kuni na kuuweka motoni, nyoka mdogo mwenye sumu akatoka kwenye zile kuni kwa sababu ya lile joto, na akajizungusha kwenye mkono wake.
4 Now when the rude people saw the venomous animal hanging from his hand, they said one to another, Surely this man is a murderer, whom though preserved from the sea, righteous vengeance suffereth not to live.
Watu wenyeji wa pale walipoona mnyama ananing'inia kutoka kwenye mkono wake, wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu hakika ni muuaji ambaye ametoroka baharini, lakini haki haimuruhusu kuishi.”
5 But he then shaking off the venomous animal into the fire, suffered no manner of inconvenience.
Lakini yeye akamtupia huyo mnyama katika moto na hakupata madhara yoyote.
6 Now they expected that a violent inflammation would ensue, or that he would have fallen suddenly dead: but when, after waiting a considerable time, they saw no inconvenience arise to him, they changed their opinion, and said that he was a divinity.
Wao walimngojea avimbe kwa homa au aanguke ghafla na kufa. Lakini baada ya kumwangalia kwa muda mrefu na kuona kwamba hakuna jambo ambalo si la kawaida kwake, walibadilisha mawazo yao na kusema alikuwa mungu.
7 Now in the vicinity of that place was the estate of the principal person on the island, named Publius, who received us into his house, and lodged us with great humanity three days.
Basi mahali pale karibu palikuwa na ardhi ambayo ilikuwa mali ya mkuu wa kisiwa, mtu aliyeitwa Pablio. Alitukaribisha na kutukarimu kwa siku tatu.
8 And it so happened that the father of Publius was then confined to his bed with an attack of fever and dysentery: unto whom Paul went in, and after praying, laid his hands upon him, and healed him.
Ilitokea kwamba baba wa Pablio alishikwa na homa na ugonjwa wa kuhara. Na Paulo alipomwendea, aliomba, akaweka mikono juu yake, na kumponya.
9 This then being the case, all the rest also who had diseases in the island came to him, and were healed.
Baada ya hili kutokea, watu wengine pale kisiwani waliokuwa wanaumwa pia walikwenda na waliponywa.
10 Then they honoured us with many tokens of respect; and when we were about to sail, laid in for us every necessary store.
Watu wakatuheshimu kwa heshima nyingi. Tulipokuwa tunajiandaa kusafiri, walitupa vile tulivyovihitaji.
11 And after three months stay we sailed in a ship which had wintered in the island, from Alexandria, whose sign was Castor and Pollux:
Baada ya miezi mitatu, tulisafiri ndani ya meli ya Iskanda ambayo ilikuwa imepigwa baridi hapo kisiwani, ambayo viongozi wake walikuwa ndugu wawili mapacha.
12 and proceeding on our voyage to Syracuse, we tarried there three days:
Baada ya kuwa tumetua katika mji wa Sirakusa, tulikaa pale siku tatu.
13 from whence we came round, and arrived opposite to Rhegium; and after one day the south wind arising, we came in two more to Puteoli:
Kutokea pale tulisafiri tukafika katika mji wa Regio. Baada ya siku moja upepo wa kusini ulitokea ghafla, na baada ya siku mbili tukafika katika mji wa Putoli.
14 where finding brethren, we were solicited by them to tarry seven days; and so we went for Rome.
Huko tuliwakuta baadhi ya ndugu na tulikaribishwa kukaa nao kwa siku saba. Kwa njia hii tukaja Rumi.
15 And the brethren from thence, when they heard of our motions, came out to meet us as far as Appii Forum and the Three Taverns: whom when Paul saw, he gave thanks to God, and felt fresh courage.
Kutoka huko wale ndugu, baada ya kuwa wamesikia habari zetu, walikuja kutupokea huko soko la Apias na Hotel tatu. Paulo alipowaona wale ndugu alimshukuru Mungu akajitia ujasiri.
16 And when we were come to Rome, the centurion delivered the prisoners to the captain of the guard; but he permitted Paul to have an apartment by himself, with a soldier only who guarded him.
Tulipoingia Roma, Paulo aliruhusiwa kuishi peke yake pamoja na yule askari aliyekuwa akimlinda.
17 Now it came to pass that after three days Paul called together the principal persons of the Jews. And when they were assembled, he said unto them, Men and brethren, though I have done nothing contrary to the people and the customs of our ancestors, yet have I been delivered up a prisoner into the hands of the Romans.
Basi ilikuwa baada ya siku tatu Paulo aliwaita pamoja wale wanume waliokuwa viongozi kati ya Wayahudi. Walipokuja pamoja, alisema kwao, “Ndugu, pamoja na kwamba sijafanya kosa lolote kwa watu hawa au kufanya kinyume na taratibu za mababa zetu waliotutangulia, nilitolewa kama mfungwa kutoka Yerusalemu hadi kwenye mikono ya Warumi.
18 Who, after a full examination, would have discharged me, because there was not the least cause found in me for death.
Baada ya kunihoji, walitamani kuniacha huru, kwa sababu kulikuwa hakuna sababu kwangu mimi ya kustahili adhabu ya kifo.
19 But when the Jews opposed it, I was constrained to appeal unto Caesar; not that I have any accusation to bring against my countrymen.
Lakini wale Wayahudi walipoongea kinyume cha shauku yao, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisaria, japokuwa haikuwa kana kwamba naleta mashtaka juu ya taifa langu.
20 For this cause therefore have I invited you hither, to see and to converse with you; for on account of the hope of Israel am I bound with this chain.
Kwa sababu ya kukata kwangu rufaa, hivyo, niliomba kuwaona na kuongea nanyi. Ni kwa sababu ya kile ambacho Israel anaujasiri kwacho, nimefungwa na kifungo hiki.
21 Then they said to him, We have neither received letters concerning thee from Judea, nor hath any one of the brethren who is arrived reported or spoken any thing evil of thee.
Kisha wakamwambia, “Hatujawahi kupokea barua kutoka Yudea kukuhusu wewe, wala hakuna ndugu aliyekuja na kutoa taarifa au kusema neno lolote baya kuhusu wewe.
22 But we think it highly proper to hear from thee what thy sentiments are; for indeed as to this sect, it is well known to us that everywhere it meets with opposition.
Lakini tunataka kusikia kutoka kwako unafikiri nini kuhusu hili kundi la watu hawa, kwa sababu inajulikana kwetu kwamba linaongea kinyume kila mahali.”
23 Then having fixed a day with him, still more of them came to him at his lodging, to whom bearing his testimony, he set forth the kingdom of God, and persuaded them of the things relating to Jesus, both out of the law of Moses and the prophets, from morning until evening:
Walipokuwa wametenga siku kwa ajili yake, watu wengi zaidi walimwijia mahali alipokuwa anaishi. Alisema lile jambo kwao na kushuhudia kuhusu ufalme wa Mungu. Alijaribu kuwashawishi kuhusu Yesu, kwa namna zote mbili kutoka katika sheria za Musa na kutoka kwa manabii, kuanzia asubuhi hadi jioni.
24 and some were convinced by the things which were spoken, but others continued in their unbelief.
Baadhi yao walishawishika kuhusu mambo yale yaliyosemwa, wakati wengine hawakuamini.
25 So being divided in sentiment among themselves, they broke up, Paul adding one word, That well had the Holy Ghost spoken by Isaiah the prophet unto our fathers,
Waliposhindwa kukubaliana wao kwa wao, waliondoka baada ya Paulo kulisema jambo hili moja, “Roho Mtakatifu alisema vyema kupitia Isaya nabii kwa baba zenu.
26 saying, Go to this people, and say, “In hearing ye shall hear, and shall not understand; and seeing ye shall see, yet in nowise perceive.
Alisema, 'Nenda kwa watu hawa useme, “Kwa masikio yenu mtasikia, lakini hamtaelewa; Na kwa macho yenu mtaona lakini hamtatambua.
27 For the heart of this people is waxed gross, and with their ears they are thick of hearing, and their eyes have they shut; lest at any time they should see with their eyes, and hear with their ears, and understand with their hearts, and become converts, and I should heal them.”
Kwa ajili ya mioyo ya watu hawa imekuwa dhaifu, masikio yao yamesikia kwa taabu, wamefumba macho yao; ili kwamba wasijekutambua kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kuelewa kwa mioyo yao, na kugeuka tena, na ningeliwaponya.”'
28 Be it known therefore unto you, that to the Gentiles is the salvation of God sent, and they will hear.
Kwa hiyo, mnapaswa kujua kwamba huu wokovu wa Mungu umepelekwa kwa watu wa Mataifa, na watasikiliza.” (Zingatia: Mstari huu
29 And when he had thus spoken, the Jews went away, and had much disputing among themselves.
“Wakati alipokuwa amesema mambo haya, wayahudi waliondoka, wakiwa na mashindano makubwa kati yao.,” haumo kwenye nakala bora za kale).
30 But Paul abode two whole years in his own hired apartment, and received all who came to him,
Paulo alikaa katika nyumba yake ya kupanga kwa miaka yote miwili, na aliwakaribisha wote waliokuja kwake.
31 preaching the kingdom of God, and teaching the things which concern the Lord Jesus Christ with all freedom of discourse, and without the least interruption.
Alikuwa akihubiri ufalme wa Mungu na alikuwa akifundisha mambo juu ya Bwana Yesu Kristo kwa ujasiri wote. Hakuna aliyemzuia.