< Acts 14 >
1 NOW it came to pass at Iconium, that they went together into the synagogue of the Jews, and spake in such a manner, as that a vast multitude both of the Jews and Greek proselytes believed.
Ikatokea ndani ya Ikonio kwamba Paulo na Barnaba waliingia pamoja ndani ya sinagogi la Wayahudi nakuongea namna ambayo kundi kubwa la watu Wayahudi na Wayunani waliamini.
2 But the unbelieving Jews stirred up, and maliciously prejudiced the spirits of the Gentiles against the brethren.
Lakini wayahudi wasiotii waliwachochea akili wamataifa na kuwafanya kuwa wabaya dhidi ya ndugu.
3 A long space therefore continued they there speaking boldly in the Lord, who bore witness to the word of his grace, and granted signs and miracles to be wrought by their hands.
Kwa hiyo walikaa huko kwa muda mrefu, wakiongea kwa ujasiri kwa nguvu ya Bwana, huku akitoa uthibitisho kuhusu ujumbe wa neema yake. Alifanya hivi kwa kutoa ishara na majaabu vifanywe kwa mikono ya Paulo na Barnaba.
4 So the multitude was divided: some indeed were with the Jews, but others with the apostles.
Lakini eneo kubwa la mji liligawanyika: baadhi ya watu walikuwa pamoja na Wayahudi, na baadhi pamoja na mitume.
5 And when there was a strong effort made both by the Gentiles and Jews with their rulers to ill-treat and stone them,
Wakati wamataifa na Wayahudi walipojaribu kuwashawishi viongozi wao kuwatendea vibaya na kuwaponda mawe Paulo na Barnaba,
6 conscious of their danger, they fled unto the cities of Lycaonia, Lystra, and Derbe, and the circum-jacent country:
wakalitambua hilo na kukimbilia katika miji ya Likaonia, Listra na Derbe, na maeneo yanayozunguka pale,
7 and there they preached the gospel.
na huko waliihubiri injili.
8 And there was a certain man at Lystra, who having lost the use of his feet was sitting, being lame from his mother’s womb, and who had never been able to walk:
Na huko Listra palikuwa na mtu mmoja aliyekaa, hakuwa na nguvu miguuni mwake, kilema kutoka tumboni mwa mama yake, hajawahi kutembea.
9 this person heard Paul speaking; who fixing his eyes on him, and discovering that he had faith to be healed,
Mtu huyu alimsikia Paulo akiongea. Paulo alimkazia macho na akaona kwamba alikuwa na imani ya kuponywa.
10 said with a loud voice, Stand up firm on thy feet! And he leaped and walked.
Hivyo alisema kwake kwa sauti ya juu, “Simama kwa miguu yako.” Na yule mtu aliruka juu na kuanza kutembea.
11 But when the multitudes beheld what Paul had done, they lifted up their voice, in the dialect of Lycaonia, saying, The gods in the form of mortals are come down to us.
Umati ulipoona alichokifanya Paulo, waliinua sauti zao, wakisema katika lahaja ya Kilikaonio, “miungu imetushukia kwa namna ya binadamu.”
12 And they called Barnabas, Jupiter; and Paul, Mercury, because he principally led the discourse.
Walimwita Barnaba “Zeu,” na Paulo “Herme” kwa sababu alikuwa msemaji mkuu.
13 Then the priest of Jupiter, who was the presiding deity of their city, brought bulls and garlands unto the gates of the city, and intended to offer a sacrifice with the people.
Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje ya mji, alileta fahari la ng'ombe na mtungo wa maua mpaka kwenye lango la mji, yeye na umati walitaka kutoa sadaka.
14 But when the apostles, Barnabas and Paul, heard it, they rent their garments, and rushed into the crowd, crying out,
Lakini mitume, Barnaba na Paulo, walipolisikia hili, walirarua mavazi yao na kwa haraka walikwenda nje kwenye umati, wakilia
15 and saying, Sirs, why do ye these things? We too are mortals subject to the same infirmities with you; preaching to you the gospel, that ye should turn from these vain things unto the living God, who made heaven, and earth, and the sea, and all things which are therein:
na kusema, “Enyi watu, kwanini mnafanya mambo haya? Na sisi pia ni binadamu wenye hisia kama za kwenu. Tunawaletea habari njema, kwamba mgeuke kutoka kwenye vitu hivi visivyofaa na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu, dunia na bahari na kila kitu kilichomo.
16 who in the past generations hath suffered all nations to walk in their own ways.
Katika nyakati zilizopita, aliwaruhusu mataifa kutembea katika njia zao wenyewe.
17 Although indeed he left not himself untestified of, doing us good, giving us from heaven showers, and fruitful seasons, replenishing our hearts with food and gladness.
Lakini bado, hakuondoka pasipo shahidi, katika hilo alifanya vizuri na akawapatia mvua kutoka mbinguni na nyakati za mazao, akiwajaza mioyo yenu kwa vyakula na furaha”
18 And thus speaking, scarce restrained they the multitudes from offering the sacrifice to them.
Hata kwa maneno haya, Paulo na Barnaba kwa shida waliuzuia umati kuwatolea sadaka.
19 Then came the Jews from Antioch and Iconium, and gaining over the multitudes, they stoned Paul, and dragged him out of the city, supposing him to be dead.
Lakini baadhi ya Wayahudi kutoka Antiokia na Ikonio walikuja kuushawishi umati. Wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji, wakidhani alikuwa amekufa.
20 But as the disciples stood around him, he arose, and entered into the city: and on the morrow he departed with Barnabas for Derbe.
Hata hivyo wanafunzi walikuwa wamesimama karibu naye, aliamka, wakaingia mjini. Siku ya pili, aliende Derbe na Barnaba.
21 And after preaching the gospel in that city, and bringing many to become disciples, they returned to Lystra, and Iconium, and Antioch;
Baada ya kufundisha injili katika mji ule na kuwafanya wanafunzi wengi, walirudi Listra, hadi Ikoniamu, na hadi Antiokia.
22 strengthening the souls of the brethren, exhorting them to abide firm in the faith, and that through many afflictions we must pass into the kingdom of heaven.
Waliendelea kuimarisha nafsi za wanafunzi na kutiwa moyo kuendelea katika imani, akasema, “Lazima tuingie katika ufalme wa Mungu kwa kupitia mateso mengi.”
23 Then appointing them presbyters in every city, by prayer with fastings they commended them to the Lord, on whom they had believed.
Walipo wateua kwa ajili yao wazee wa kila kusanyiko la waaminio, na wakiwa wameomba na kufunga, waliwakabidhi kwa Bwana, ambaye wao walimwamini.
24 Then passing through Pisidia, they came unto Pamphylia.
Kisha walipita katika Pisidia, walifika Pamfilia.
25 And having spoken the word in Perga, they went down to Attalia:
Wakati walipoongea maneno katika Perga, waliteremka kwenda Atalia.
26 and thence sailed for Antioch, from whence they had been commended to the grace of God for the service which they had performed.
Kutoka huko walipanda meli hadi Antiokia ambako walikuwa wamejitoa kwa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameikamilisha.
27 So when they arrived they called the church together, and related what great things God had done by them, and that he had opened to the heathen the door of faith.
Walipofika huko Antiokia, na kulikusanya kusanyiko la pamoja, wakatoa taarifa ya mambo ambayo Mungu amefanya kwao, na jinsi alivyowafungulia mlango wa imani kwa watu wa Mataifa.
28 And there they abode no inconsiderable time with the disciples.
Walikaa kwa muda mrefu na wanafunzi.