< Acts 13 >
1 NOW there were at Antioch, according to the established church, prophets and teachers; such as Barnabas, and Simeon called Niger the black, and Lucius a Cyrenian, and Manaen, Herod the tetrarch’s foster-brother, and Saul.
Sasa katika kanisa la Antiokia, palikuwa na baadhi ya manabii na walimu. Walikua Barnaba, Simeoni (aliyeitwa Nigeri). Lukio wa Kirene, Manaeni( ndugu asiye wa damu wa Herode kiongozi wa mkoa), na Sauli.
2 And as they were employed in the ministry, and kept a fast, the Holy Ghost said, Set apart for me now both Barnabas and Saul for the work whereunto I have called them.
Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema, “Niteengeeni pembeni Barnaba na Sauli, waifanye kazi niliyo waitia.”
3 Then having kept a fast and prayed, and laid their hands on them, they sent them out.
Baada ya Kanisa kufunga, kuomba, na kuweka mikono yao juu ya watu hawa, wakawaacha waende.
4 They then being sent forth indeed by the Holy Ghost, went down to Seleucia; and from thence sailed to Cyprus.
Kwa hiyo Barnabas na Sauli walimtii Roho Mtakatifu na walitelemka kuelekea Seleukia; Kutoka huko walisafiri baharini kuelekea kisiwa cha Kipro.
5 And being at Salamis, they preached the word of God in the synagogues of the Jews: and they had John also as their attendant.
Walipokuwa katika mji wa Salami, walilitangaza neno la Mungu katika Masinagogi ya Wayahudi. Pia walikuwa pamoja na Yohana Marko kama msaidizi wao.
6 Now as they travelled through the island as far as Paphos, they found a certain person who professed magic, a false prophet, a Jew, whose name was Bar-jesus:
Walipokwenda katika kisiwa chote mpaka Pafo, walikuta mtu fulani mchawi, Myahudi nabii wa uongo, ambaye jina lake lilikuwa Bar Yesu.
7 who was with the proconsul Sergius Paulus, an intelligent man; he inviting to his house Barnabas and Saul, desired earnestly to hear the word of God.
Mchawi huyu alishirikiana na Liwali Sergio Paulus, aliyekuwa mtu mwenye akili. Mtu huyu aliwaalika Barnaba na Sauli, kwa sababu alihitaji kusikia neno la Mungu.
8 But Elymas the magician (for such is his name when interpreted) opposed them, seeking to pervert the proconsul from the faith.
Lakini Elima “yule mchawi” (hivyo ndivyo jina lake lilivyo tafsiriwa) aliwapinga; alijaribu kumgeuza yule liwali atoke kwenye imani.
9 Then Saul (now Paul), filled with the Holy Ghost, and fixing his eyes upon him,
Lakini Sauli aliyeitwa Paulo, alikuwa amejazwa na Roho Mtakatikfu, akamkazia macho
10 said, O thou full of all guile and all mischief, thou child of the devil, thou enemy of all righteousness, wilt thou not cease perverting the strait ways of the Lord?
na akasema “Ewe mwana wa Ibilisi, umejazwa na aina zote za udanganyifu na udhaifu. Wewe ni adui wa kila aina ya haki. Hautakoma kuzigeuza njia za Bwana, zilizonyooka, je utaweza?
11 And now, behold, the hand of the Lord is upon thee, and thou shalt be blind, seeing the sun no more for a season. And instantly there fell on him a thick mist and darkness; and groping about he sought some to lead him by the hand.
Sasa tazama, mkono wa Bwana upo juu yako, na utakuwa kipofu. Hautaliona Jua kwa muda” mara moja ukungu na giza vilianguka juu ya Elimas; alianza kuzunguka pale akiomba watu wamwongoze kwa kumshika mkono.
12 Then when the proconsul saw what was done, he believed, being struck with the doctrine of the Lord.
Baada ya liwali kuona kilichotokea, aliamini, kwa sababu alishangazwa kwa mafundisho kuhusu Bwana.
13 Hereupon sailing from Paphos, they who were about Paul came to Perga in Pamphylia: but John departing from them returned to Jerusalem.
Sasa Paulo na rafiki zake walisafiri majini kutoka Pafo na wakafika Perge katika Pamfilia. Lakini Yohana aliwaacha na kurudi Yerusalemu.
14 And they departed from Perga, and came to Antioch in Pisidia, and entering into the synagogue on the sabbath-day, they sat down.
Paulo na rafiki yake walisafiri kutoka Perge na wakafika Antiokia ya Pisidia. Huko walikwenda katika sinagogi siku ya Sabato na kukaa chini.
15 Then after the reading of the law and the prophets, the rulers of the synagogues sent to them, saying, Men and brethren, if ye are disposed to give a word of exhortation to the people, speak.
Baada ya kusoma sheria na manabii, viongozi wa sinagogi aliwatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mnao ujumbe wa kutia moyo watu hapa, semeni”
16 Then Paul arose, and waving his hand, said, Men of Israel, and ye that fear God, hear me.
Kwa hiyo Paulo alisimama na kuwapungia mkono; alisema, “Wanaume wa Israeli na enyi mnao mtii Mungu, sikilizeni.
17 The God of this people Israel selected our fathers, and exalted the people during their abode in the land of Egypt, and with a mighty arm brought he them out of it.
Mungu wa hawa watu wa Israeli aliwachagua baba zetu na kuwafanya watu wengi walipokaa katika nchi Misri, na kwa mkono wake kuinuliwa aliwaongoza nje yake.
18 And about the space of forty years he bore with their behaviour in the wilderness.
Kwa miaka arobaini aliwavumilia katika jangwa.
19 And destroying seven nations in the land of Canaan, he distributed their territory to them by lot.
Baada ya kuyaharibu mataifa saba katika nchi ya Kaanani, aliwapa watu wetu nchi yao kwa urithi.
20 And after these things, during a space of about four hundred and fifty years, he gave them judges until Samuel the prophet.
Matukio haya yote yalitokea zaidi ya miaka mia nne na hamsini. Baada ya vitu hivi vyote, Mungu aliwapa waamuzi mpaka Samweli Nabii.
21 And from that time they desired a king: and God gave them Saul the son of Kis, a man of the tribe of Benjamin, during forty years.
Baada ya haya, watu waliomba mfalme, hivyo Mungu aliwapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila la Benjamini, kuwa mfalme kwa miaka arobaini.
22 And removing him, he raised up unto them David to be king; respecting whom also he spake testifying, “I have found David the son of Jesse, a man after my own heart, who shall perform all my intentions.”
Kisha baada ya Mungu kumuondoa katika ufalme, alimwinua Daudi kuwa mfalme wao. Ilikuwa ni kuhusu Daudi kwamba Mungu alisema, 'Nimempata Daudi mwana wa Yese kuwa mtu apendezwaye na moyo wangu; ambaye atafanya kila kitu nipendacho.'
23 From this man’s seed according to the promise hath God raised up to Israel a Saviour, Jesus:
Kutoka kwenye ukoo wa mtu huyu Mungu ameiletea Israeli mkombozi, Yesu, kama alivyoahidi kufanya.
24 John having preached before his first coming the baptism of repentance to all the people of Israel.
Hili lilianza kutokea, kabla ya Yesu kuja, Yohana kwanza alitangaza ubatizo wa toba kwa watu wote wa Israeli.
25 But as John was finishing his course, he said, Whom do ye suppose me to be? I am not the Messiah. But, behold! he is coming after me, the sandals of whose feet I am not worthy to loose.
Naye Yohana alipokuwa akimalizia kazi yake, alisema, 'Mwanifikiri mimi ni nani? mimi si yule. Lakini sikilizeni, ajaye nyuma yangu, sisitahili kulegeza viatu vya miguu yake.'
26 Men and brethren, children of the race of Abraham, and all among you who fear God, to you is the word of this salvation sent.
Ndugu, watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wale ambao kati yenu mnamwabudu Mungu, ni kwa ajili yetu kwamba ujumbe huu wa ukombozi umetumwa.
27 For they who dwell at Jerusalem, and their rulers, being ignorant of him, and the words of the prophets that are read every sabbath-day, by condemning him have fulfilled them.
Kwa wale waishio Yerusalemu, na watawala wao, hawakumtambua kwa uhalisia, na wala hawakuutambua ujumbe wa manabii ambao husomwa kila Sabato; kwa hiyo walitimiliza ujumbe wa manabii kwa kumhukumu kifo Yesu.
28 And though they found no cause of death in him, they besought Pilate that he might be killed.
Japokuwa hawakupata sababu nzuri kwa kifo ndani yake, walimwomba Pilato amuue.
29 But when they had finished all things that were written of him, they took him down from the tree, and laid him in a sepulchre.
Walipomaliza mambo yote yaliyoandikwa kuhusu yeye, walimshusha kutoka mtini na kumlaza kaburini.
30 But God raised him from the dead:
Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31 and he was seen many days by those who went up with him from Galilee to Jerusalem, who are his witnesses to the people.
Alionekana kwa siku nyingi kwa wale waliokwenda pamoja naye kutoka Galilaya kuelekea Yerusalemu. Watu hawa sasa ni mashahidi wa watu.
32 And we preach to you the promise made to our fathers;
Hivyo tunawaletea habari njema kuhusu ahadi walizopewa mababu zetu.
33 for this hath God fulfilled to their children, even to us, in raising up Jesus: as it is also written in the second Psalm, “Thou art my Son, this day have I begotten thee.”
Mungu aliweka ahadi hizi kwetu, watoto wao, katika hilo alimfufua Yesu na kumrudisha tena katika uhai. Hili pia liliandikwa katika Zaburi ya pili: 'Wewe ni Mwanangu, leo nimekuwa Baba yako'
34 But that he raised him from the dead, no more in future to return to corruption, he hath thus spoken, “I will give you the holy things of David, which are sure.”
Pia kuhusu ukweli ni kwamba alimfufua kutoka wafu ili kwamba mwili wake usiharibike, ameongea hivi: 'Nitakupatia utakatifu na baraka halisi za Daudi'
35 Wherefore also he saith in another place, “Thou wilt not permit thy Holy One to see corruption.”
Hii ndiyo sababu kasema pia katika zaburi nyingine, 'Hautaruhusu mtakatifu wako kuuona uozo.'
36 For David indeed, after having served his own generation by the will of God, fell asleep, and was placed with his fathers, and saw corruption.
Kwa kuwa baada ya Daudi kutumikia mapenzi ya Mungu katika kizazi chake, alilala, alilazwa pamoja na baba zake, na aliuona uaharibifu,
37 But he, whom God raised up, saw no corruption.
Lakini aliyefufuliwa na Mungu hakuuona uharibifu.
38 Be it therefore known unto you, men and brethren, that through this man remission of sin is proclaimed to you:
Hivyo na ifahamike kwenu, ndugu, kupitia mtu huyu, msamaha wa dhambi umehubiriwa.
39 and by this man shall every one who believeth be justified from all things, from which it was not possible that he should be justified by the law of Moses.
Kwa yeye kila aaminiye anahesabiwa haki na mambo yote ambayo sheria ya Musa isingewapatia haki.
40 Take heed then, that this come not upon you, which is spoken by the prophets;
Hivyo basi kuweni waangalifu kwamba kitu walichokiongelea manabii kisitokee kwenu:
41 “Behold, ye despisers, and wonder, and perish: for I do a work in your days, a work which ye shall in no wise believe, though one declare it unto you.”
'Tazama, enyi mnaodharau, na mkashangae na mkaangamie; kwa vile nafanya kazi katika siku zenu, Kazi ambayo hamwezi kuiamini, hata kama mtu atawaeleza.”
42 But when the Jews were going out of the synagogue, the Gentiles entreated that these words might be spoken to them the following sabbath.
Wakati Paulo na Barnaba walipoondoka, watu wakawaomba waongee maneno haya siku ya Sabato ijayo.
43 And when the synagogue was dismissed, many of the Jews and of the devout proselytes followed Paul and Barnabas: who, exhorting them, persuaded them to abide stedfast in the grace of God.
Wakati mkutano wa sinagogi ulipokwisha, Wayahudi wengi na waongofu thabiti waliwafuata Paulo na Barnaba, ambao waliongea nao na waliwahimiza waendelee katika neema ya Mungu.
44 And on the next sabbath almost all the city thronged together to hear the word of God.
Sabato iliyofuata, karibu mji mzima ulikusanyika kusikia neno la Mungu.
45 But the Jews seeing the multitude, were filled with envy, and opposed the things spoken by Paul, contradicting and reviling.
Wayahudi walipoona makutano, walijawa na wivu na kuongea maneno yaliyopinga vitu vilivyosemwa na Paulo na walimtukana.
46 Then Paul and Barnabas speaking with undaunted boldness, said, It was necessary that the word of God should be first spoken unto you: but since ye have thrust it from you, and judged yourselves not worthy of eternal life, lo! we turn to the Gentiles. (aiōnios )
Lakini Paulo na Barnaba waliongea kwa ujasiri na kusema, “Ilikuwa ni muhimu kwamba neno la Mungu liongelewe kwanza kwenu. Kwa kuwa mnalisukumia mbali kutoka kwenu nakujiona kuwa hamkusitahili uzima wa milele, angalieni tutawageukia Mataifa. (aiōnios )
47 For so hath the Lord enjoined us, “I have set thee for a light of the Gentiles, that thou mightest be for salvation unto the extremity of the earth.”
Kama ambavyo Bwana ametuamuru, akisema, 'Nimewaweka ninyi kama nuru kwa watu wa mataifa, kwamba mlete wokovu kwa pande zote za dunia.”
48 Now when the Gentiles heard this, they rejoiced, and glorified the word of the Lord: and they believed, even as many as were ordained to life eternal. (aiōnios )
Mataifa waliposikia hili, walifurahi na kulisifu neno la Bwana. Wengi waliochaguliwa kwa uzima wa milele waliamini. (aiōnios )
49 So the word of the Lord was diffused through the whole region.
Neno la Bwana lilienea nchi yote.
50 Then the Jews stirred up the devout women, and those who were respectable, and the principal persons of the city, and raised up a persecution against Paul and Barnabas, and cast them out of their borders.
Lakini wayahudi waliwasihi waliojitoa na wanawake muhimu, pia na viongozi wa mji. Haya yalichochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na waliwatupa nje ya mipaka ya mji.
51 But they, shaking off the dust of their feet against them, came to Iconium.
Lakini Paulo na Barnaba walikung'uta vumbi ya miguu yao. Kisha walienda kwenye mji wa Ikonia.
52 And the disciples were filled with joy, and with the Holy Ghost.
Na wanafunzi walijawa na furaha pamoja na Roho mtakatifu.