< Psalms 60 >

1 To him that excelleth upon Shushan Eduth, or Michtam. A Psalme of David to teach. When he fought against Aram Naharaim, and against Aram Zobah, when Joab returned and slew twelve thousand Edomites in the salt valley. O God, thou hast cast vs out, thou hast scattered vs, thou hast bene angry, turne againe vnto vs.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Shushani Eduthi.” Utenzi wa Daudi wa kufundisha. Wakati alipopigana na Waaramu kutoka Aramu-Naharaimu na Aramu-Soba, naye Yoabu akarudi nyuma na kuwaua Waedomu 12,000 katika Bonde la Chumvi. Ee Mungu, umetukataa na kutokea ghafula juu yetu, umekasirika: sasa turejeshe upya!
2 Thou hast made the land to tremble, and hast made it to gape: heale the breaches thereof, for it is shaken.
Umetetemesha nchi na kuipasua; uiponye mavunjiko yake, kwa maana inatetemeka.
3 Thou hast shewed thy people heauy things: thou hast made vs to drinke the wine of giddines.
Umewaonyesha watu wako nyakati za kukata tamaa; umetunywesha mvinyo unaotuyumbisha.
4 But now thou hast giuen a banner to them that feare thee, that it may be displayed because of thy trueth. (Selah)
Kwa wale wanaokucha wewe, umewainulia bendera, ili iweze kutwekwa dhidi ya upinde.
5 That thy beloued may be deliuered, helpe with thy right hand and heare me.
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
6 God hath spoken in his holines: therefore I will reioyce: I shall deuide Shechem, and measure the valley of Succoth.
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
7 Gilead shalbe mine, and Manasseh shalbe mine: Ephraim also shalbe the strength of mine head: Iudah is my lawgiuer.
Gileadi ni yangu na Manase ni yangu; Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
8 Moab shalbe my wash pot: ouer Edom will I cast out my shoe: Palestina shew thy selfe ioyfull for me.
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
9 Who will leade me into the strong citie? who will bring me vnto Edom?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
10 Wilt not thou, O God, which hadest cast vs off, and didest not go forth, O God, with our armies?
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
11 Giue vs helpe against trouble: for vaine is the helpe of man.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
12 Through God we shall doe valiantly: for he shall tread downe our enemies.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.

< Psalms 60 >