< Numbers 31 >

1 And the Lord spake vnto Moses, saying,
BWANA alinena na Musa na kumwambia,
2 Reuenge the children of Israel of the Midianites, and afterwarde shalt thou be gathered vnto thy people.
“Uwalipizie kisasi Wamidiani kwa kile walichowafanya Waisraeli. Baada ya kufanya hivyo utakufa na kukusanyika na watu wako.”
3 And Moses spake to the people, saying, Harnesse some of you vnto warre, and let them goe against Midian, to execute the vengeance of the Lord against Midian.
Kwa hiyo Musa akawaambia watu. Akasema, “andaeni baadhi ya majeshi yenu kwa ajili ya vita ili kwamba wakawapige Wamidiani na kubeba kiapo cha BWANA.
4 A thousande of euery tribe throughout all the tribes of Israel, shall ye sende to the warre.
Kwa kila kabila la Israeli watatuma askari elfu moja kwa ajili ya vita.”
5 So there were taken out of the thousands of Israel, twelue thousande prepared vnto warre, of euery tribe a thousand.
Kwa hiyo kati ya wanaume maelfu elfu wa Israeli, wanaume elfu moja walitolewa kwa ajili ya vita, jumla ya wanaume elfu kumi na mbili.
6 And Moses sent them to the warre, euen a thousand of euery tribe, and sent them with Phinehas the sonne of Eleazar the Priest to the warre: and the holy instruments, that is, the trumpets to blow were in his hand.
Kisha Musa akawatuma kwenda vitani, elfu moja toka kila kabila pamoja na Finehasi mwana wa Eliazari kuhanai, wakiwa na vitu kutoka mahali patakatifu wakiwa na matarumbeta kwa ajili ya ishara za sauti.
7 And they warred against Midian, as the Lord had commanded Moses, and slue all the males.
Wakapigana na Midiani, kama BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa. Wakamwua kila mwanaume.
8 They slue also the Kings of Midian among them that were slaine: Eui and Rekem, and Zur, and Hur and Reba fiue kings of Midian, and they slue Balaam the sonne of Beor with the sworde:
Wakawaua wafalme wa Midiani pamoja na wengine waliowaua ni: Evi, Rekimu, Zuri, Huri, na Reba, hawa walaikuwa ndio waflme watano wa Midiani. pia walimwua Balaamu mwana wa Beori, kwa upanga.
9 But the children of Israel tooke the women of Midian prisoners, and their children, and spoyled all their cattell, and all their flockes, and all their goods.
Jeshi la Israeli likawachukua mateka wanawake wa Midiani, watoto wao, mifugo yao yote, kondoo wao na bidhaa zao zote. walivichukua hivi kama mateka.
10 And they burnt all their cities, wherein they dwelt, and all their villages with fire.
Waliichoma moto miji yao yote walimoishi na kambi zao zote.
11 And they tooke all the spoyle and all the pray both of men and beastes.
Walichukua vitu vyote na wafungwa, watu na wanyama.
12 And they brought the captiues and that which they had taken, and the spoyle vnto Moses and to Eleazar the Priest, and vnto the Congregation of the children of Israel, into ye campe in the playne of Moab, which was by Iorden toward Iericho.
Wakawaleta mateka, nyara, na wakakamata vitu wakavileta kwa Musa, na Eliazari kuhani, na kwa jamii ya watu wa Israeli. Wakavileta hivi vitu kambini katika uwanda wa Moabu, kule Yorodani karibu na Yeriko.
13 Then Moses and Eleazar the Priest, and all the princes of the Congregation went out of the campe to meete them.
Musa, Eliazari kuhani, pamoja na viongozi wa watu wakaenda kukutana nao nje ya kambi.
14 And Moses was angry with the captaines of the hoste, with the captaines ouer thousands, and captaines ouer hundreds, which came from the warre and battel.
Lakini Musa alikuwa na hasira dhidi ya viongozi wa jeshi, Wale majemedari wa maelfu na maakida wa mamia, waliotoka kupigana.
15 And Moses sayde vnto them, What? haue ye saued all the women?
Musa akawaambia, “Je, mmeawaacha wanawake wote kuishi?
16 Behold, these caused the children of Israel through the counsell of Balaam to commit a trespasse against the Lord, as concerning Peor, and there came a plague among the Congregation of the Lord.
Tazama, wanawake hawa ndio waliosababisha watu wa Israeli, kwa kupitia ushauri wa Balaamu, kufanya dhambi dhidi ya BWANA huko Peori, wakati ile tauni iliposambaa kwa watu wa Mungu.
17 Now therefore, slay all the males among the children, and kill all the women that haue knowen man by carnall copulation.
Sasa basi, ueni kila mwanaume kuanzia wadogo, na ueni kila mwanamke aliyelala na mwanamume.
18 But all the women children that haue not knowen carnall copulation, keepe aliue for your selues.
Lakini chukueni wale mabinti wadogo ambao hawajalala na mwanamume.
19 And ye shall remaine without the host seuen dayes, all that haue killed any person, and all that haue touched any dead, and purifie both your selues and your prisoners the third day and the seuenth.
Mtaweka kambi nje na kambi za Israeli kwa muda wa siku saba. Ninyi wote ambao mmeua watu au ambao mmegusa maiti yeyote mtajitakasa wenyewe katika siku ya tatu na katika siku ya saba - ninyi na mateka wenu.
20 Also ye shall purifie euery garment and all that is made of skins and al worke of goates heare, and all things made of wood.
Na mtayatakasa mavazi yenu yote, na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi za wanyama, na manyoya ya mbuzi, na kila kitu kilichotengenezwa kwa mbao.”
21 And Eleazar ye Priest sayd vnto the men of warre, which went to the battel, This is the ordinance of the law which the Lord commanded Moses,
Eliazarai kuahani akawaambia wale wanajeshi waliokuwa wameenda vitani, “Hii ni amri ya sheria ambayo BWANA alimpa Musa:
22 As for gold, and siluer, brasse, yron, tynne, and lead:
Zile dhahabu, fedha, vyuma, bati, risasi,
23 Euen all that may abide the fire, yee shall make it goe through the fire, and it shalbe cleane: yet, it shalbe purified with the water of purification: and all that suffereth not the fire, yee shall cause to passe by the water.
na kila kitu knaweza kuhhimili moto, mtakiweka katka moto, navyo vitakuwa safi. Nakisha mtavitakasa vitu hivyo na maji ya farakano. Na vitu vyote ambavyo haviwezi kupita katika moto, mtavitakasa kwa maji hayo.
24 Ye shall wash also your clothes the seuenth day, and ye shalbe cleane: and afterward ye shall come into the Hoste.
Na mtazifua nguao zenu katika siku ya saba, ndipo mtakapokuwa safi. Baada ya hapo mnaweza kurudi kwenye kambi za Israeli.”
25 And the Lord spake vnto Moses, saying,
Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,
26 Take the summe of the praie that was taken, both of persons and of cattell, thou and Eleazar the Priest, and the chiefe fathers of the Congregation.
“Vihesabu vitu vyote vilivyochukuliwa nyara, wote watu na wanyama. Wewe, Eliazari kuhani, na viongozi wa watu kufuata koo
27 And deuide the praye betweene the souldiers that went to the warre, and all the Congregation.
watavigawa hivi vitu katika mkundi mawili. Mvigawe kwa wanajeshi walioenda kupigana na kwa watu wote.
28 And thou shalt take a tribute vnto ye Lord of the men of warre, which went out to battel: one person of fiue hundreth, both of the persons, and of the beeues, and of the asses, and of the sheepe.
Kisha toza kodi ambayo itatolewa kwangu kutoka kwa wanajeshi waliokuwa wameenda vitani. Hii kodi itakuwa moja kati ya mia tano, katika watu, ng'ombe, punda, kondoo, au mbuzi.
29 Yee shall take it of their halfe and giue it vnto Eleazar the Priest, as an heaue offring of the Lord.
Uichukue hii kodi kutoka katika nusu yao na umpe Eliazari kuhani kwa ajili ya sadaka itakayotolewa kwangu.
30 But of the halfe of the children of Israel thou shalt take one, taken out of fiftie, both of the persons, of the beeues, of the asses, and of the sheepe, euen of all the cattel: and thou shalt giue them vnto the Leuites, which haue the charge of the Tabernacle of the Lord.
Pia kutoka katika nusu ya watu wa Israeli, utachukua moja kati ya hamsini -kutoka vitu, ng'ombe, punda, na mbuzi. Uvitoe hivi kwa Walawi wanaotumika katika masikani yangu.”
31 And Moses and Eleazar the priest did as the Lord had commanded Moses.
Kwa hiyo Musa na Eliazari kuhani wakafanya kama BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa.
32 And the bootie, to wit, the rest of the praie which the men of warre had spoyled, was sixe hundreth seuentie and fiue thousand sheepe,
Sasa zile nyara zilizokuwa zimebaki ambazo wanajeshi walikuwa wameteka zilikuwa kondoo 675, 000,
33 And seuentie and two thousand beeues,
maksai elfu sabini na mbili,
34 And three score and one thousand asses,
punda elfu sitini na moja,
35 And two and thirtie thousande persons in all, of women that had lyen by no man.
na wanawake elfu thelathini na mbili ambao walikuwa hawajalala na mwanamume yeyote.
36 And the halfe, to wit, the part of them that went out to warre touching the nomber of sheepe, was three hundreth seuen and thirtie thousand, and fiue hundreth.
Ile hesabu ya nusu iliyokuwa imetunzwa kwa ajili ya wanajeshi ilikuwa kondoo 337, 000. Ile sehemu ya
37 And the Lordes tribute of the sheepe was sixe hundreth and seuentie and fiue:
BWANA ya kondoo ilikuwa kondoo 675.
38 And the beeues were six and thirty thousad, whereof the Lordes tribute was seuentie and two.
Maksai walikuwa elfu thelathini na sita ambayo kodi ya BWANA ilikuwa sabini na mbili.
39 And the asses were thirtie thousande and fiue hundreth, whereof the Lordes tribute was three score and one:
Punda walikuwa 30, 500 ambao sehemu ya BWANA ilikuwa sitini na moja.
40 And of persons sixtene thousand, whereof the Lordes tribute was two and thirtie persons.
Watu walikuwa wanawake elfu kumi na sita ambao kodi ya BWANA ilikuwa thelathini na mbili.
41 And Moses gaue the tribute of the Lordes offring vnto Eleazar the Priest, as the Lord had commanded Moses.
Musa aliichukua ile kodi ambayo ilitakiwa kuwekwa sadaka kwa BWANA. Akampatia Eliazari kuhani, kama BWANA alivyomwamuru Musa.
42 And of the halfe of the children of Israel, which Moses deuided from the men of warre,
Ile nusu ya watu wa Israeli ambayo Musa alikuwa ameichukua toka kwa wanawjeshi waliokuwa wameenda vitani -
43 (For the halfe that perteined vnto the Congregation, was three hundreth thirtie and seuen thousand sheepe and fiue hundreth,
ile nusu y a watu ilikuwa kondoo 337, 500,
44 And sixe and thirtie thousand beeues,
maksai elfu thelathini na sita,
45 And thirtie thousand asses, and fiue hudreth,
punda 30, 500,
46 And sixteene thousande persons)
na wanawake elfu kumi na sita.
47 Moses, I say, tooke of the halfe that perteined vnto the children of Israel, one taken out of fiftie, both of the persons, and of the cattell, and gaue them vnto the Leuites, which haue the charge of the Tabernacle of the Lord, as the Lord had commanded Moses.
Kutoka kwenye nusu ya watu wa Israeli, Musa alichukua moja katika hamsini, wote watu na wanyama. Aliwapa Walawi ambao huitumikia masikani ya BWANA, kama BWANA alivyokuwa amemwamuru kufanya.
48 Then the captaines which were ouer thousandes of the hoste, the captaines ouer the thousandes, and the captaines ouer the hundreds came vnto Moses:
Kisha wale maakida wa jeshi, makamanda wa elfu na makapteni wa mamia, wakaja kwa Musa.
49 And saide to Moses, Thy seruants haue taken the summe of the men of warre which are vnder our authoritie, and there lacketh not one man of vs.
Wakamwambia, “watumishi wako wamewahesabu wanajeshi ambao wako chini yetu, hakuna hata mmoja wao aliyekosa.
50 We haue therefore brought a present vnto the Lord, what euery man found of iewels of golde, bracelets, and cheines, rings, eare ringes, and ornaments of the legges, to make an atonement for our soules before the Lord.
Tumemletea BWANA sadaka, ambayo kila mmoja amepata, vitu vya dhahabu, metali, timbi, pete za mhuri, vipini na vikuku, ili kujifanyia upatanisho kwa BWANA.”
51 And Moses and Eleazar the Priest tooke the golde of them, and all wrought iewels,
Musa na Eliazari kuhani akapokea kutoka kwao dhahabu na vitu vyote vilivyotengenezwa kwa ufundi.
52 And all the golde of the offring that they offered vp to the Lord (of the captaines ouer thousands and hundreds) was sixteene thousande seuen hundreth and fiftie shekels,
Vitu vyote vya sadaka ya dhahabu ambavyo walimpa BWANA- sadaka toka kwa makamanda wa maelfu na kutoka kwa makepteni wa mamia - vilikuwa na uzito wa shekeli 16, 750.
53 (For the men of warre had spoyled, euery man for him selfe)
Kila mwanajeshi alikuwa ameteka nyara ya kila mtu kwa ajili yake.
54 And Moses and Eleazar the Priest tooke the golde of the captaines ouer the thousandes, and ouer the hundreds, and brought it into the Tabernacle of the Congregation, for a memoriall of the children of Israel before the Lord.
Musa na Eliazari kuhani wakazichukuazile dhahabu toka kwa makamanda wa maelfu na makepteni wa mamia. Wakavipeleka kwenye hema ya kukutania kama ukumbusho wa watu wa Israeli kwa BWANA.

< Numbers 31 >