< Matthew 21 >

1 And when they drewe neere to Hierusalem, and were come to Bethphage, vnto the mount of the Oliues, then sent Iesus two disciples,
Yesu na wanafunzi wake wakafika karibu na Jerusalemu na wakaenda mpaka Bethfage, katika mlima mizeituni, kisha Yesu akawatuma wanafunzi wawili,
2 Saying to them, Goe into the towne that is ouer against you, and anon yee shall finde an asse bounde, and a colt with her: loose them, and bring them vnto me.
akiwaambia, “Nendeni katika kijiji kinachofuata, na mara moja mtamkuta punda amefungwa pale, na mwanapunda pamoja naye. wafungueni na kuwaleta kwangu.
3 And if any man say ought vnto you, say ye, that the Lord hath neede of them, and straightway he will let them goe.
Ikiwa mtu yeyote akiwaambia chochote kuhusu hilo, mtasema, `Bwana anawahitaji, ` na mtu huyo mara moja atawaruhusu mje pamoja nao”
4 All this was done that it might be fulfilled, which was spoken by the Prophet, saying,
Jambo hili lilitokea ni lile lililosemwa kupitia kwa nabii lazima litimizwe. Akawaambia,
5 Tell ye the daughter of Sion, Beholde, thy King commeth vnto thee, meeke and sitting vpon an asse, and a colte, the foale of an asse vsed to the yoke.
Waambie binti Sayuni, tazama, mfalme wako anakuja kwenu, mnyenyekevu na akiwa amempanda punda, na mwana punda mme, mwana punda mchanga.
6 So the disciples went, and did as Iesus had commanded them,
Kisha wanafunzi waliondoka na kufanya kama Yesu alivyowaagiza.
7 And brought the asse and the colt, and put on them their clothes, and set him thereon.
Wakamleta punda na mwanapunda, na kuweka nguo zao juu yao, naye Yesu akakaa pale.
8 And a great multitude spred their garments in the way: and other cut downe branches from the trees, and strawed them in the way.
Wengi katika mkusanyiko walitandaza nguo zao njiani, na wengine walikata matawi kutoka kwenye miti na kutandaza barabarani.
9 Moreouer, the people that went before, and they also that followed, cried, saying, Hosanna to the Sonne of Dauid, Blessed be hee that commeth in the Name of the Lord, Hosanna thou which art in the highest heauens.
Umati uliomtangulia Yesu na wale waliomfuata walipaza sauti, wakisema,”Hosana kwa mwana wa Daudi! Ni mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana. Hosana juu zaidi!”
10 And when he was come into Hierusalem, all the citie was mooued, saying, Who is this?
Yesu alipofika Yerusalemu, mji mzima ulishtuka na kusema, “Huyu ni nani?
11 And the people said, This is Iesus that Prophet of Nazareth in Galile.
“Umati ulijibu, “Huyu ni Yesu Nabii, kutoka Nazareti ya Galilaya.”
12 And Iesus went into the Temple of God, and cast out all them that solde and bought in the Temple, and ouerthrew the tables of the money chagers, and the seates of them that sold doues,
Kisha Yesu akaingia katika hekalu la Mungu. akawafukuza nje wote waliokuwa wakinunua na kuuza hekaluni. Pia alipindua meza za wabadilishaji wa fedha na viti vya wauza njiwa.
13 And said to them, it is written, My house shall be called the house of prayer: but ye haue made it a denne of theeues.
Akawaambia, “Imeandikwa, `'Nyumba yangu itaitwa nyumba ya maombi, `lakini ninyi mmeifanya pango la wanyang`anyi.”
14 Then the blinde, and the halt came to him in the Temple, and he healed them.
kisha vipofu na vilema wakamjia hekaluni, naye akawaponya.
15 But when the chiefe priestes and Scribes sawe the marueiles that hee did, and the children crying in the Temple, and saying, Hosanna to the Sonne of Dauid, they disdained,
Lakini wakati wakuu wa makuhani na waandishi walipoona maajabu aliyoyatenda, na waliposikia watoto wakipiga kelele hekaluni na kusema, “Hosana kwa Mwana wa Daudi,” walishikwa na hasira.
16 And said vnto him, Hearest thou what these say? And Iesus said vnto them, Yea: read ye neuer, By the mouth of babes and sucklings thou hast made perfite the praise?
Wakamwambia, “Umesikia kile kinachosemwa na hawa watu?” Yesu akawaambia, “Ndiyo! Lakini hamjawahi kusoma, 'Kutoka kwa midomo ya watoto na watoto wachanga wanyonyao mna sifa kamili?''
17 So hee left them, and went out of the citie vnto Bethania, and lodged there.
Kisha Yesu akawaacha na kwenda nje ya mji katika Bethania na kulala huko.
18 And in the morning, as he returned into the citie, he was hungrie,
Asubuhi alipokuwa anarudi mjini, alikuwa na njaa.
19 And seeing a figge tree in the way, he came to it, and found nothing thereon, but leaues onely, and said to it, Neuer fruite grow on thee henceforwards. And anon the figge tree withered. (aiōn g165)
Aliona mtini kandokando ya barabara. Akauendea, lakini hakupata kitu juu yake isipokuwa majani. Aliuambia, “Kusiwe na matunda kwako daima tena.” Na mara hiyo mtini ule ukanyauka. (aiōn g165)
20 And when his disciples saw it, they marueiled, saying, How soone is the figge tree withered!
Wanafunzi walipoona, wakastaajabu na kusema, “Imekuwaje mtini umenyauka mara moja?”
21 And Iesus answered and said vnto them, Verely I say vnto you, if ye haue faith, and doubt not, ye shall not only doe that, which I haue done to the figge tree, but also if ye say vnto this mountaine, Take thy selfe away, and cast thy selfe into the sea, it shalbe done.
Yesu akajibu na kuwaambia, “Kweli nawaambieni, kama mkiwa na imani na bila wasiwasi, hamtafanya kile kilichofanyika kwa huo mtini tu, lakini mtauambia hata huo mlima, ` uchukuliwe na ukatupwe baharini, `na itafanyika.
22 And whatsoeuer ye shall aske in prayer, if ye beleeue, ye shall receiue it.
Chochote mtakachoomba kwa sala, huku mkiamini, mtapokea.”
23 And whe he was come into the Temple, the chiefe Priestes, and the Elders of the people came vnto him, as he was teaching, and saide, By what authoritie doest thou these things? and who gaue thee this authoritie?
Yesu alipofika hekaluni, wakuu wa makuhani na wazee wa watu wakamjia wakati alipokuwa akifundisha na kumwuliza, “Ni kwa mamlaka gani unafanya mambo haya? Na ni nani aliyekupa mamlaka haya?”
24 Then Iesus answered and said vnto them, I also will aske of you a certaine thing, which if ye tell me, I likewise will tell you by what authoritie I doe these things.
Yesu akajibu na kuwaambia, “Nami tena nitawauliza swali moja. kama mkiniambia, nami vilevile nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
25 The baptisme of Iohn, whence was it? from heauen, or of men? Then they reasoned among themselues, saying, If we shall say, From heauen, he will say vnto vs, Why did ye not then beleeue him?
Ubatizo wa Yohana- ulitoka wapi, mbinguni au kwa wanadamu?” Wakahojiana wenyewe, wakisema, tukisema, ulitoka mbinguni, `atatuambia, kwa nini hamkumwamini? `
26 And if we say, Of men, we feare the multitude, for all holde Iohn as a Prophet.
Lakini tukisema, `ulitoka kwa wanadamu, `tunawaogopa makutano, kwa sababu wote wanamwona Yohana kama nabii.”
27 Then they answered Iesus, and said, We can not tell. And he said vnto them, Neither tell I you by what authoritie I doe these things.
Kisha wakamjibu Yesu na kusema, “Hatujui” Akawaambia pia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani nafanya mambo haya.
28 But what thinke ye? A certaine man had two sonnes, and came to the elder, and saide, Sonne, goe and worke to day in my vineyarde.
Lakini mnafikiri nini? Mtu mwenye wana wawili. Akaenda kwa moja na kumwambia, `Mwanangu, nenda ukafanye kazi katika shamba la mizabibu
29 But he answered, and said, I will not: yet afterward he repented himselfe, and went.
leo. `Mwana akajibu na kusema, `sitakwenda, ' Lakini baadaye akabadilisha mawazo yake na akaenda.
30 Then came he to the second, and said likewise. And he answered, and said, I will, Syr: yet he went not.
Na Mtu yule akaenda kwa mwana wa pili na kusema kitu kilekile. Mwana huyu akajibu na kusema, `nitakwenda, bwana', lakini hakwenda.
31 Whether of them twaine did the will of the father? They saide vnto him, The first. Iesus saide vnto them, Verely I say vnto you, that the Publicanes and the harlots goe before you into the kingdome of God.
Yupi kati ya wana wawili aliyefanya matakwa ya baba yake? Wakasema, “Mwana wa kwanza.” Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, wakusanya ushuru na makahaba wataingia kwenye ufalme wa Mungu kabla yenu kuingia.
32 For Iohn came vnto you in the way of righteousnes, and yee beleeued him not: but the Publicanes, and the harlots beleeued him, and ye, though ye sawe it, were not mooued with repentance afterward, that ye might beleeue him.
Kwa maana Yohana alikuja kwenu kwa njia iliyo nyoofu, lakini hamkumwamini, wakati wakusanya ushuru na makahaba walimwamini. Na ninyi, mlipoona hilo likitendeka, hamkuweza kutubu ili baadaye mumwamini.
33 Heare another parable, There was a certaine housholder, which planted a vineyard, and hedged it round about, and made a winepresse therein, and built a tower, and let it out to husbandmen, and went into a strange countrey.
Sikilizeni mfano mwingine. Kulikuwa na mtu, mtu mwenye eneo kubwa la ardh. Alipanda mizabibu, akaiwekea uzio, akatengeneza na chombo cha kukamlia divai, akajenga na mnara wa walinzi, na akalikodisha kwa watunza zabibu. Kisha akaenda katika nchi nyingine.
34 And when the time of the fruite drewe neere, hee sent his seruants to the husbandmen to receiue the fruites thereof.
Wakati wa mavuno ya mizabibu ulipokaribia, aliwatuma baadhi ya watumishi kwa wakulima wa mizabibu kuchukua mizabibu yake.
35 And ye husbandmen tooke his seruants and beat one, and killed another, and stoned another.
Lakini wakulima wa zabibu wakawachukua watumishi wake, wakampiga mmoja, wakamwua mwingine, na wakampiga mmoja kwa mawe.
36 Againe hee sent other seruants, moe then the first: and they did the like vnto them.
Kwa mara nyingine, Mmiliki aliwatuma watumishi wengine, wengi zaidi ya wale wa kwanza, lakini wakulima wa mizabibu waliwatendea vilevile.
37 But last of all he sent vnto them his owne sonne, saying, They will reuerence my sonne.
Baada ya hapo bwana yule akamtuma kwao mwana wake, akisema, `'Watamheshimu mwanangu.'`
38 But when the husbandmen saw the sonne, they saide among themselues, This is the heire: come, let vs kill him, and let vs take his inheritance.
Lakini wakulima wa mizabibu walipomwona kijana yule, wakaambizana, `'Huyu ni mrithi, Njooni, tumuue na tumiliki urithi.'
39 So they tooke him, and cast him out of the vineyarde, and slewe him.
`Hivyo wakamchukua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu na kumwua.
40 When therefore the Lord of the vineyarde shall come, what will hee doe to those husbandmen?
Je mmliki wa shamba la mizabibu atakapokuja, atawafanya nini wakulima wa mizabibu?”
41 They saide vnto him, Hee will cruelly destroy those wicked men, and will let out his vineyard vnto other husbandmen, which shall deliuer him the fruites in their seasons.
Wakamwambia, “Atawaharibu hao watu waovu katika njia ya ukali zaidi, na kisha atalikodisha shamba la mizabibu kwa wakulima wengine wa mizabibu, watu ambao watalipa kwa ajili ya mizabibu itakapoiva.”
42 Iesus saide vnto them, Read ye neuer in the Scriptures, The stone which the builders refused, the same is made the head of the corner? This was the Lordes doing, and it is marueilous in our eyes.
Yesu akawaambia, “Hamkusoma katika maandiko, 'Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la msingi. Hili lilitoka kwa Bwana, na inashangaza machoni petu?'
43 Therefore say I vnto you, The kingdome of God shalbe taken from you, and shalbe giuen to a nation, which shall bring foorth the fruites thereof.
Hivyo nawaambieni, Ufalme wa Mungu utatwaliwa kutoka kwenu na kupewa taifa linalojali matunda yake.
44 And whosoeuer shall fall on this stone, he shalbe broken: but on whomsoeuer it shall fall, it will dash him a pieces.
Yeyote atakayeanguka juu ya jiwe hilo atavunjwa vipandevipande. Lakini kwa yeyote litakayemwangukia, litamsaga.”
45 And when the chiefe Priestes and Pharises had heard his parables, they perceiued that hee spake of them.
Wakuu wa makuhani na mafarisayo waliposikia mifano yake, wakaona kuwa anawazungumzia wao.
46 And they seeking to laye handes on him, feared the people, because they tooke him as a Prophet.
Lakini kila walipotaka kunyosha mikono juu yake, waliogopa makutano, kwa sababu watu walimtazama kama nabii.

< Matthew 21 >