< Leviticus 10 >

1 But Nadab and Abihu, the sonnes of Aaron, tooke either of them his censor, and put fire therein, and put incense thereupon, and offred strange fire before the Lord, which hee had not commanded them.
Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua vyetezo vyao, wakaweka moto ndani yake na kuongeza uvumba; kisha wakamtolea Bwana moto usio halali, kinyume na agizo la Mungu.
2 Therefore a fire went out from the Lord, and deuoured them: so they dyed before the Lord.
Hivyo moto ukaja kutoka kwa uwepo wa Bwana na kuwaramba, nao wakafa mbele za Bwana.
3 Then Moses sayde vnto Aaron, This is it that the Lord spake, saying, I will bee sanctified in the that come neere me, and before all the people I will be glorified: but Aaron held his peace.
Kisha Mose akamwambia Aroni, “Hili ndilo alilonena Bwana wakati aliposema: “‘Miongoni mwa wale watakaonikaribia nitajionyesha kuwa mtakatifu; machoni pa watu wote nitaheshimiwa.’” Aroni akanyamaza.
4 And Moses called Mishael and Elzaphan the sonnes of Vzziel, the vncle of Aaron, and saide vnto them, Come neere, cary your brethre from before the Sanctuarie out of the hoste.
Mose akawaita Mishaeli na Elisafani, wana wa Uzieli mjomba wake Aroni, akawaambia, “Njooni hapa. Ondoeni miili ya binamu zenu mbele ya mahali patakatifu, mkaipeleke nje ya kambi.”
5 Then they went, and caried them in their coates out of the host, as Moses had comaunded.
Hivyo wakaja na kuwaondoa, wakiwa bado wamevalia makoti yao ya ibada, wakawapeleka nje ya kambi, kama Mose alivyoamuru.
6 After, Moses saide vnto Aaron and vnto Eleazar and Ithamar his sonnes, Vncouer not your heads, neither rent your clothes, least ye dye, and least wrath come vpon all ye people: but let your brethren, all the house of Israel bewayle the burning which the Lord hath kindled.
Ndipo Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe, Eleazari na Ithamari, “Msifunue vichwa vyenu wala msirarue mavazi yenu, la sivyo mtakufa na Bwana ataikasirikia jumuiya nzima. Lakini ndugu zenu, nyumba yote ya Israeli, wanaweza kuwaombolezea wale ambao Bwana amewaangamiza kwa moto.
7 And go not yee out from the doore of the Tabernacle of the Congregation, least ye dye: for the anointing oyle of the Lord is vpon you: and they did according to Moses commandement.
Msitoke nje ya ingilio la Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa, kwa sababu mafuta ya Bwana ya upako yako juu yenu.” Hivyo wakafanya kama vile Mose alivyosema.
8 And the Lord spake vnto Aaron, saying,
Kisha Bwana akamwambia Aroni,
9 Thou shalt not drinke wine nor strong drinke, thou, nor thy sonnes with thee, when yee come into the Tabernacle of the Congregation, lest ye die: this is an ordinance for euer throughout your generations,
“Wewe na wanao msinywe mvinyo wala kinywaji kingine kilichochachuka wakati mwingiapo katika Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa. Hili litakuwa Agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo.
10 That ye may put difference betweene the holy and the vnholy, and betweene the cleane and the vncleane,
Ni lazima mtenganishe kilicho kitakatifu na kile kilicho cha kawaida, kati ya yaliyo najisi na yaliyo safi,
11 And that ye may teach the children of Israel all the statutes which the Lord hath commanded them by the hand of Moses.
na lazima mwafundishe Waisraeli amri zote ambazo Bwana aliwapa kupitia Mose.”
12 Then Moses saide vnto Aaron and vnto Eleazar and to Ithamar his sonnes that were left, Take the meate offring that remaineth of the offrings of the Lord, made by fire, and eate it without leauen beside ye altar: for it is most holy:
Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe waliosalia, Eleazari na Ithamari, “Chukueni sadaka ya nafaka iliyobaki kutoka sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, muile hapo kando ya madhabahu ikiwa imeandaliwa bila chachu, kwa sababu ni takatifu sana.
13 And ye shall eate it in the holy place, because it is thy duetie and thy sonnes duety of the offringes of the Lord made by fire: for so I am commanded.
Mtaila katika mahali patakatifu kwa sababu ni fungu lenu na fungu la wana wenu la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, kwa maana hivyo ndivyo nilivyoamriwa.
14 Also the shaken breast and the heaue shoulder shall yee eate in a cleane place: thou, and thy sonnes, and thy daughters with thee: for they are giuen as thy duetie and thy sonnes duety, of the peace offringes of the children of Israel.
Lakini wewe na wanao na binti zako mwaweza kula kidari kile kilichoinuliwa na paja lile lililotolewa. Mtavila mahali safi pa kawaida ya ibada; mmepewa wewe na watoto wako kuwa fungu lenu la sadaka za amani za Waisraeli.
15 The heaue shoulder, and the shaken breast shall they bring with the offringes made by fire of the fat, to shake it to and from before the Lord, and it shalbe thine and thy sonnes with thee by a lawe for euer, as the Lord hath commanded.
Paja lile lililotolewa na kidari kile kilichoinuliwa lazima viletwe pamoja na sehemu za mafuta ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, ili kuinuliwa mbele za Bwana kama sadaka ya kuinuliwa. Hili litakuwa fungu lako la kawaida na wanao, kama Bwana alivyoagiza.”
16 And Moses sought the goate that was offred for sinne, and lo, it was burnt: therefore he was angrie with Eleazar and Ithamar the sonnes of Aaron, which were left aliue, saying,
Mose alipouliza kuhusu mbuzi atolewaye kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kukuta kwamba ameteketezwa, aliwakasirikia Eleazari na Ithamari, wana wa Aroni waliobaki, akawauliza,
17 Wherfore haue ye not eaten the sinne offring in the holy place, seeing it is most Holie? and God hath giuen it you, to beare the iniquitie of the Congregation, to make an atonement for them before the Lord.
“Kwa nini hamkula sadaka ya dhambi katika eneo la mahali patakatifu? Ni takatifu sana. Mlipewa ninyi ili kuondoa hatia ya jumuiya kwa ajili ya kuwafanyia upatanisho mbele za Bwana.
18 Beholde, the blood of it was not brought within the holy place: ye should haue eaten it in the holy place, as I commanded.
Kwa kuwa damu yake haikuletwa ndani ya Mahali Patakatifu, mngemla mbuzi huyo katika sehemu ya mahali patakatifu kama nilivyoagiza.”
19 And Aaron said vnto Moses, Behold, this day haue they offred their sinne offring, and their burnt offring before the Lord, and such things as thou knowest are come vnto mee: If I had eaten the sinne offring to day, should it haue bene accepted in the sight of the Lord?
Aroni akamjibu Mose, “Leo wanangu wametoa sadaka zao za dhambi na sadaka zao za kuteketezwa mbele za Bwana, lakini mambo kama haya yamenitokea mimi. Je, Bwana angependezwa kama ningekuwa nimekula sadaka ya dhambi leo?”
20 So when Moses heard it, he was content.
Mose aliposikia haya, akaridhika.

< Leviticus 10 >