< Jeremiah 51 >
1 Thus sayth the Lord, Beholde, I wil raise vp against Babel, and against the inhabitants that lift vp their heart against me, a destroying wind,
Yahwe asema hivi: Tazama, ninakwenda kuleta upepo wa maangamizi dhidi ya Babeli na dhidi yao waishio ndani ya Leb Kamei.
2 And wil send vnto Babel fanners that shall fanne her, and shall empty her land: for in the day of trouble they shalbe against her on euery side.
Nitawatuma Babeli wageni. Watamtawanya na wataifanya ukiwa nchi yake, maana watakuja kinyume chake kutoka pote siku ya madhara.
3 Also to the bender that bendeth his bowe, and to him that lifteth himselfe vp in his brigandine, will I say, Spare not her yong men, but destroy all her hoste.
Msiwaache wapiga mishale wakapinda pinde zao; msiwache wakavaa silaha zao. Msiwahifadhi vijana wake wa kiume; litengeni jeshi lake lote kwa maangamizi.
4 Thus the slaine shall fall in the lande of the Caldeans, and they that are thrust through in her streetes.
Maana watu waliojeruhiwa wataanguka katika nchi ya Wakaldayo; waliouawa wataanguka katika mitaa yake.
5 For Israel hath bene no widowe, nor Iudah from his God, from the Lord of hostes, though their lande was filled with sinne against the holy one of Israel.
Maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, na Yahwe wa majeshi, japokuwa nchi yao imejaa na maasi yaliyotendwa kinyume cha Mmoja aliye Mtakatifu wa Israeli.
6 Flee out of the middes of Babel, and deliuer euery man his soule: be not destroyed in her iniquitie: for this is the time of the Lordes vengeance he will render vnto her a recompence.
Kimbieni kutoka Babeli; kila mtu na ajiokoe mwenyewe. Msiangamie katika maasi yake. Maana ni wakati wa kisasi cha Yahwe. Atamlipa kwa yote.
7 Babel hath bene as a golden cuppe in the Lordes hand, that made all the earth drunken: the nations haue drunken of her wine, therefore do the nations rage.
Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yahwe kilichoinywesha nchi yote; mataifa walikunywa mvinyo wake wakawa wendawazimu.
8 Babel is suddenly fallen, and destroyed: howle for her, bring balme for her sore, if she may be healed.
Babeli utaanguka ghafla na kuangamizwa. Mwombolezeeni! mpeni dawa kwa maumivu yake; pengine aweza kupona.
9 We would haue cured Babel, but she could not be healed: forsake her, and let vs go euery one into his owne countrey: for her iudgement is come vp vnto heauen, and is lifted vp to ye cloudes.
Tulinuia kumponya Babeli, lakini hajaponywa, haya na tumwache twende, katika nchi yetu. Maana hatia yake imefika juu mbinguni; imerundikwa kufika mawinguni.
10 The Lord hath brought forth our righteousnesse: come and let vs declare in Zion the worke of the Lord our God.
Yahwe ametamka kwamba sisi hatuna hatia. Njooni, teseme katika Sayuni matendo ya Yahwe Mungu wetu.'
11 Make bright the arrowes: gather the shieldes: the Lord hath raised vp the spirit of the King of the Medes: for his purpose is against Babel to destroy it, because it is the vengeance of the Lord, and the vengeance of his Temple.
Noweni mishale na kuchukua ngao. Yahwe anaiimiza roho ya mfalme wa Umedi katika mpango wa kuiangamiza Babeli. Hii ni kwa kisasi cha Yahwe, kisasi kwa maangamizi ya hekalu lake.
12 Set vp the standart vpon the walles of Babel, make the watch strong: set vp the watchmen: prepare the skoutes: for the Lord hath both deuised, and done that which he spake against the inhabitantes of Babel.
Inueni bendela juu ya kuta za Babeli; wekeni walinzi. Wekeni waangalizi; wekeni askari waviziao ili kumkamata kila akimbiliaye mjini, maana Yahwe atafanya kile alichokipanga. Atafanya alichokisema juu ya wakaao Babeli.
13 O thou that dwellest vpon many waters, abundant in treasures, thine ende is come, euen the ende of thy couetousnes.
Enyi mwishio kati ya chemchemi nyingi za maji, ninyi mlio na wingi wa hazina, mwisho wenu umefika. upindo wa maisha yenu umepunguzwa.
14 The Lord of hostes hath sworne by him selfe, saying, Surely I will fill thee with men, as with caterpillers, and they shall cry and shoute against thee.
Yahwe wa majeshi ameapa kwa maisha yake, 'nitakujaza na adui zako, kama pigo la nzige; watainua kelele za vita juu yako.'
15 He hath made the earth by his power, and established the world by his wisedome, and hath stretched out the heauen by his discretion.
Ameifanya dunia kwa nguvu zake; akaiweka dunia mahali kwa hekima yake. Kwa ufahamu wake alizitanda mbingu.
16 Hee giueth by his voyce the multitude of waters in the heauen, and he causeth the cloudes to ascend from the endes of the earth: he turneth lightnings to raine, and bringeth forth the winde out of his treasures.
Anapovuma, kunakuwa na mvumo wa maji mbinguni, maana huleta umande kutoka miisho ya dunia. Hufanya radi kwa ajili ya mvua na kuituma na kuutuma upepo kutoka katika maghala ya nyumba zake.
17 Euery man is a beast by his owne knowledge: euery founder is confounded by the grauen image: for his melting is but falsehood, and there is no breath therein.
Kila mtu anakuwa kama mnyama asiye na akili; kila mfua chuma ameaibishwa na sanamu zake. Maana mwonekano wake unadanganya; maana hakuna uzima ndani yake.
18 They are vanitie, and the worke of errours: in the time of their visitation they shall perish.
Hazifai, kazi ya wafanya mzaa; wataangamizwa wakati wa kuadhibiwa kwao.
19 The portion of Iaakob is not like them: for he is the maker of all things, and Israel is the rodde of his inheritance: the Lord of hostes is his Name.
Lakini Mungu, urithi wa Yakobo, siyo kama hawa, maana yeye ndiye afanyaye vitu vyote. Israeli ni kabila ya urithi wake; Yahwe wa majeshi ni jina lake.
20 Thou art mine hammer, and weapons of warre: for with thee will I breake the nations, and with thee wil I destroy kingdomes,
Wewe ni nyundo ya vita yao, silaha ya vita yangu. Kwa wewe nitawaponda mataifa na kuharibu falme.
21 And by thee wil I breake horse and horseman, and by thee will I breake the charet and him that rideth therein.
Kwa wewe nitaponda farasi na wawapandao; kwa wewe nitaponda vibandawazi na madereva wake.
22 By thee also will I breake man and woman, and by thee wil I breake olde and yong, and by thee wil I breake the yong man and the mayde.
Kwa wewe nitawafutilia mbali mme na mke; kwa wewe nitafutilia mbali mzee na kijana. Kwa wewe nitafutilia mbali kijana wa kiume na wasichana bikra.
23 I wil also breake by thee the shepheard and his flocke, and by thee will I breake the husband man and his yoke of oxen, and by thee will I breake the dukes and princes.
Kwa wewe nitafutilia mbali wachungaji na makundi yao; kwa wewe nitawafutilia mbali wakulima na jozi zao za kulimia. kwa wewe nitawafutilia mbali watawala na maafsa.
24 And I will render vnto Babel, and to all the inhabitants of the Caldeans all their euil, that they haue done in Zion, euen in your sight, sayth the Lord.
Maana mbele yako nitamlipa Babeli na wote wakaao Ukaldayo kwa maovu yote waliyoyafanya huko Sayuni - hili ni tamko la Yahwe.
25 Beholde, I come vnto thee, O destroying mountaine, sayth the Lord, which destroyest all the earth: and I will stretch out mine hand vpon thee, and rolle thee downe from the rockes, and wil make thee a burnt mountaine.
Tazama, mimi ni kinyume chako, ewe mlima, wewe unayewaharibu watu wengine - hili ni tamko la Yahwe - kuiharibu dunia yote. Nitakupiga na mikono yangu na kuvingirisha chini kutoka ukingo wa kilima. Kisha nitakufanya mlima ulioteketezwa kabisa kwa moto.
26 They shall not take of thee a stone for a corner, nor a stone for foundations, but thou shalt be destroyed for euer, sayth the Lord.
Hivyo hawatachukua kwako jiwe lolote ili kujengea pembe ya nyumba au msingi; kwani utakuwa ukiwa wa milele - hili ni tamko la Yahwe.
27 Set vp a standard in the lande: blowe the trumpets among the nations: prepare the nations against her: call vp the kingdomes of Ararat, Minni, and Ashchenaz against her: appoynt the prince against her: cause horses to come vp as the rough caterpillers.
Inua bendela ya vita juu ya nchi. Piga tarumbeta katika mataifa. Yaite mataifa yamshambuliye: Ararati, Mini na Ashkenazi. Teua majemedari wa kumshambulia; leta farasi kama nzige warukao.
28 Prepare against her the nations with the Kings of the Medes, the dukes thereof, and the princes thereof, and all the land of his dominion.
Waandae mataifa kumshambulia: wafalme wa Umedi na magavana wao, maafsa wake wote na nchi yake yete.
29 And the land shall tremble and sorow: for the deuise of the Lord shalbe performed against Babel, to make the lande of Babel waste without an inhabitant.
Maana nchi itatikisika na kudhoofika, kwa kuwa mipango ya Yahwe inaendelea juu ya Babeli, kuifanya nchi ya Babeli kuwa nchi isiyofaa mahali pasipo na mtu.
30 The strong men of Babel haue ceased to fight: they haue remayned in their holdes: their strength hath fayled, and they were like women: they haue burnt her dwelling places, and her barres are broken.
Maaskari wameacha kupigana huko Babeli; wamekaa katika ngome zao. Nguvu zao zimeshindwa; wamekuwa wanawake - nyumba zake zipo motoni, makomeo ya malango yake yamevunjika.
31 A post shall runne to meete the post, and a messenger to meete the messenger, to shew the King of Babel, that his citie is taken on a side thereof,
Mjumbe hukimbia ili amwambie mjumbe mwingine, na mtoa habari humwambia mtoa habari mwingine ili amwambie mfalme wa Babeli kwamba mji wake umetwaliwa kutoka mwisho hata mwisho.
32 And that the passages are stopped, and the reedes burnt with fire, and the me of war troubled.
Hivyo vivuko katika mito vimekamatwa; adui anaunguza mafunjo ya bwawa, na wapiganaji wa Babeli wamechanganyikiwa.
33 For thus sayth the Lord of hosts the God of Israel, the daughter of Babel is like a threshing floore: the time of her threshing is come: yet a litle while, and the time of her haruest shall come.
Maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria. Ni muda wa kumkanyaga. Ni kitambo kidogo wakati wa mavuno utakuja juu yake.
34 Nebuchad-nezzar the King of Babel hath deuoured me, and destroyed me: he hath made me an emptie vessel: he swallowed mee vp like a dragon, and filled his belly with my delicates, and hath cast me out.
Yerusalemu husema, 'Nebukadneza mfalme wa Babeli amenirarua. Amenikausha na amenifanya kuwa mtungi mtupu. Amenimeza kama joka. Alijishibisha kwa chakula changu chema. Amenitupa mbali.'
35 The spoyle of me, and that which was left of me, is brought vnto Babel, shall the inhabitant of Zion say: and my blood vnto the inhabitantes of Caldea, shall Ierusalem say.
Wenyeji wa Sayuni watasema, 'Gasia nilizofanyiwa na mwili wangu na ziwe kwa Babeli.' Yerusalem atasema, Damu yangu na iwe juu ya wakaao Ukaldayo.'
36 Therefore thus sayth the Lord, Beholde, I will maintayne thy cause, and take vengeance for thee, and I will drie vp the sea, and drie vp her springes.
Kwa hiyo Yahwe asema hivi: Tazama, nikotayari kulitetea shitaka lako na kuleta kisasi kwa ajili yako. Maana nitayakausha maji ya Babeli na kufanya vyanzo vyake kukauka.
37 And Babel shall be as heapes, a dwelling place for dragons, an astonishment, and an hissing, without an inhabitant.
Babeli utakuwa rundo la magofu, pango la mbwea, sehemu itishayo, kitu cha kutoa sauti ya nyoka, pasipo na watu.
38 They shall rore together like lions, and yell as the lyons whelpes.
Wababeli wataunguruma kwa pamoja kama wanasimba. Watanguruma kama watoto wa simba.
39 In their heate I will make them feastes, and I wil make them drunken, that they may reioyce, and sleepe a perpetual sleepe, and not wake, sayth the Lord.
wanapopashwa moto kwa hasira, nitawafanyia sherehe; nitawalewesha hata wafurahi, na kisha kulala usingizi usio na mwisho hata wasiamke - hili ni tamko la Yahwe -
40 I wil bring them downe like lambes to the slaughter, and like rams and goates.
nitawapeleka chini kama wanakondoo kwa mchinjaji, kama kondoo dume pamoja na mbuzi majike.
41 How is Sheshach taken! and howe is the glory of the whole earth taken! how is Babel become an astonishment among the nations!
Jinsi Babeli ulivyotekwa! Hivyo fahari ya dunia yote imekamatwa. Jinsi Babeli ulivyofanyika sehemu yenye magofu kati ya mataifa.
42 The sea is come vp vpon Babel: he is couered with the multitude of the waues thereof.
Bahari imekuja juu ya Babeli! Amefunikwa na mawimbi yavumayo.
43 Her cities are desolate: the land is dry and a wildernes, a land wherein no man dwelleth, neither doth the sonne of man passe thereby.
Miji yake imekuwa ukiwa, sehemu kame na nyika, nchi isiyo na watu, na hakuna mtu apitaye hapo.
44 I wil also visite Bel in Babel, and I wil bring out of his mouth, that which he hath swallowed vp, and the nations shall runne no more vnto him, and the wall of Babel shall fall.
Hivyo nitamwadhibu Beli huko Babeli; nitakitoa kinywani mwake alichokimeza, na mataifa hawatamminikia tena pamoja na wazao wao. Kuta za Babeli zitaanguka.
45 My people, go out of the middes of her, and deliuer yee euery man his soule from the fierce wrath of the Lord,
Tokeni kati yake, enyi watu wangu. Kila mmoja wenu aokowe maisha yake kutoka katika hasira ya gadhabu yangu.
46 Least your heart euen faynt, and ye feare the rumour, that shalbe heard in the land: the rumour shall come this yeere, and after that in the other yeere shall come a rumour, and crueltie in the land, and ruler against ruler.
Msiache mioyo yenu ikaogopa au kuhofu habari iliyosikiwa nchini, maana habari itakuja siku moja. Baada yake mwaka unaofuata kutakuwa na habari, na ghasia zitakuwa nchini. Mtawala atakuwa kinyume cha mtawala.
47 Therefore beholde, the dayes come, that I will visite the images of Babel, and the whole land shalbe confounded, and all her slayne shall fall in the middes of her.
Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja nitakapoadhibu sanamu za Babeli. Nchi yake yote itaaibika, na wote waliochinjwa wataanguka ndani yake.
48 Then the heauen and the earth, and all that is therein, shall reioyce for Babel: for the destroyers shall come vnto her from the North, saith the Lord.
Kisha mbingu na nchi, na vyote vilivyomo ndani yake vitafurahi juu ya Babeli. Maana mwalibifu atamwijia kutoka kaskazini - hili ni tamko la Yahwe.
49 As Babel caused the slaine of Israel to fal, so by Babel the slaine of all the earth did fall.
“Kama Babeli alivyowafanya waliouawa wa Israeli kuanguka, hivyo waliouawa katika nchi yake wataanguka katika Babeli.
50 Ye that haue escaped the sworde, goe away, stand not still: remember the Lord a farre of, and let Ierusalem come into your minde.
Ondokeni!, manusura wa vita, Msikawiye. Mkumbukeni Yahwe tokea mbali; Yerusalemu na ikumbukwe.
51 Wee are confounded because wee haue heard reproch: shame hath couered our faces, for straungers are come into the Sanctuaries of the Lordes House.
Tumeaibika, maana tumesikia matusi; dhihaka imefunika nyuso zetu, maana wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Yahwe.
52 Wherefore behold, the dayes come, sayth the Lord, that I will visite her grauen images, and through all her land the wounded shall grone.
Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - nitakapoziadhibu sanamu zake, na waliojeruhiwa watanung'unika kwa maumivu katika nchi yake yote.
53 Though Babel should mount vp to heauen, and though shee should defend her strength on hye, yet from mee shall her destroyers come, sayth the Lord.
Maana hata kama Babeli angepanda mbinguni au kujenga ngome zake ndefu, aharibuye kutoka kwangu angemwendea - hili ni tamko la Yahwe.
54 A sound of a cry commeth from Babel, and great destruction from the land of the Caldeans,
Kelele ya maangamizi ilitoka Babeli, anguko kubwa kutoka nchi ya Wakaldayo.
55 Because the Lord hath layde Babel waste and destroyed from her the great voyce, and her waues shall roare like great waters, and a sounde was made by their noyse:
Maana Yahwe anaiharibu Babeli. Anaifanya kelele ya sauti yake kuisha. Adui zake wanaunguruma kama mawimbi ya maji mengi; kelele yao imekuwa na nguvu.
56 Because the destroyer is come vpon her, euen vpon Babel, and her strong men are taken, their bowes are broken: for the Lord God that recompenceth, shall surely recompence.
Maana aharibuye amekuja kinyume chake - kinyume cha Babeli! - na shujaa wake wametekwa. Pinde zao zimevunjwa, maana Yahwe ni Mungu wa kisasi; atatekeleza kisasi hiki.
57 And I will make drunke her princes, and her wise men, her dukes, and her nobles, and her strong men: and they shall sleepe a perpetuall sleepe, and not wake, sayth the King, whose Name is the Lord of hostes.
Maana nitawafanya wana wafalme wake, wenye hekima wake, maofsa wake, na maaskari wake kulewa, nao watalala usingizi kwa usingizi usioisha na bila kuamka - hili ni tamko la mfalme: Yahwe wa majeshi ndilo jina lake.
58 Thus saith the Lord of hostes, The thicke wall of Babel shalbe broken, and her hie gates shall be burnt with fire, and the people shall labour in vaine, and the folke in ye fire, for they shalbe weary.
Yahwe wa majeshi asema hivi: Ukuta mnene wa Babeli utaangushwa kabisa, na malango marefu yataunguzwa. Kisha watu wanaokuja kumsaidia watafanya kazi isiyofaa; kila mataifa wanachojaribu kikifanya kwa ajili yake kitateketezwa kwa moto.”
59 The worde which Ieremiah the Prophet commanded Sheraiah the sonne of Neriiah, the sonne of Maaseiah, when he went with Zedekiah the King of Iudah into Babel, in the fourth yeere of his reigne: and this Sheraiah was a peaceable prince.
Hili ndilo neno Yeremia nabii alilomwamru Seraya mwana wa Neria mwana wa Makseya alipokwenda na Sedekia mfalme wa Yuda huko Babeli katika mwaka wa nne wa kutawala kwake. Basi Seraya alikuwa afsa mwandamizi.
60 So Ieremiah wrote in a booke all the euill that should come vpon Babel: euen al these things, that are written against Babel.
Maana Yeremia alikuwa ameandika katika gombo kuhusu madhara yote yeliyokuwa yakienda kutendeka juu ya Babeli - maneno haya yote yaliyokuwa yameandikwa juu ya Babeli
61 And Ieremiah sayd to Sheraiah, Whe thou commest vnto Babel, and shalt see, and shalt reade all these wordes,
Yeremia akamwambia Seraya, “Unapokwenda Babeli, hakikisha unayasoma maneno haya yote.
62 Then shalt thou say, O Lord, thou hast spoken against this place, to destroy it, that none should remaine in it, neither man nor beast, but that it should be desolate for euer.
Nawe utasema, 'Yahwe, wewe! - wewe mwenyewe umesema kwamba utapaharibu mahali hapa. Hapatakuwa na wa kukaa, kwamba ni watu au wanyama. Patakuwa nchi isiyofaa daima.'
63 And when thou hast made an ende of reading this booke, thou shalt binde a stone to it, and cast it in the middes of Euphrates,
Kisha mtakapomaliza kusoma gombo hili, funga jiwe kubwa juu yake na ulitupe katikati ya Frati.
64 And shalt say, Thus shall Babel be drowned, and shall not rise from the euil, that I will bring vpon her: and they shall be weary. Thus farre are the wordes of Ieremiah.
Sema, 'Babeli utazama kama hivi. Hautainuka kwa sababu ya mabaya ninayoyapeleka juu yake, nao wataanguka.” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.