< Hosea 10 >
1 Israel is a emptie vine, yet hath it brought foorth fruite vnto it selfe, and according to the multitude of the fruite thereof he hath increased the altars: according to the goodnesse of their lande they haue made faire images.
Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana, alijizalia matunda mwenyewe. Kadiri matunda yake yalivyoongezeka, alijenga madhabahu zaidi; kadiri nchi yake ilivyostawi, alipamba mawe yake ya ibada.
2 Their heart is deuided: nowe shall they be founde faultie: he shall breake downe their altars: he shall destroy their images.
Moyo wao ni mdanganyifu, nao sasa lazima wachukue hatia yao. Bwana atabomoa madhabahu zao na kuharibu mawe yao ya ibada.
3 For now they shall say, We haue no King because we feared not the Lord: and what should a King doe to vs?
Kisha watasema, “Hatuna mfalme kwa sababu hatukumheshimu Bwana. Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme, angeweza kutufanyia nini?”
4 They haue spoken woordes, swearing falsly in making a couenant: thus iudgement groweth as wormewoode in the furrowes of the fielde.
Wanaweka ahadi nyingi, huapa viapo vya uongo wanapofanya mapatano; kwa hiyo mashtaka huchipuka kama magugu ya sumu katika shamba lililolimwa.
5 The inhabitants of Samaria shall feare because of the calfe of Beth-auen: for the people thereof shall mourne ouer it, and the Chemarims thereof, that reioyced on it for the glorie thereof, because it is departed from it.
Watu wanaoishi Samaria huogopa kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni. Watu wake wataiombolezea, vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu, wale waliokuwa wamefurahia fahari yake, kwa sababu itaondolewa kutoka kwao kwenda uhamishoni.
6 It shall bee also brought to Asshur, for a present vnto King Iareb: Ephraim shall receiue shame, and Israel shall be ashamed of his owne counsell.
Itachukuliwa kwenda Ashuru kama ushuru kwa mfalme mkuu. Efraimu atafedheheshwa; Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
7 Of Samaria, the King thereof is destroyed as the some vpon the water.
Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya uso wa maji.
8 The hie places also of Auen shall be destroied, euen the sinne of Israel: the thorne and the thistle shall growe vpon their altars, and they shall say to the mountaines, Couer vs, and to the hils, Fall vpon vs.
Mahali pa kuabudia sanamu pa uovu pataharibiwa: ndiyo dhambi ya Israeli. Miiba na mibaruti itaota na kufunika madhabahu zao. Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!” na vilima, “Tuangukieni!”
9 O Israel, thou hast sinned from the daies of Gibeah: there they stoode: the battell in Gibeah against the children of iniquitie did not touch them.
“Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli, huko ndiko mlikobaki. Je, vita havikuwapata watenda mabaya huko Gibea?
10 It is my desire that I should chastice them, and the people shall be gathered against them, when they shall gather themselues in their two furrowes.
Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu; mataifa yatakusanywa dhidi yao ili kuwaweka katika vifungo kwa ajili ya dhambi zao mbili.
11 And Ephraim is as an heifer vsed to delite in threshing: but I will passe by her faire necke: I will make Ephraim to ride: Iudah shall plowe, and Iaakob shall breake his cloddes.
Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa ambaye hupenda kupura, hivyo nitamfunga nira juu ya shingo yake nzuri. Nitamwendesha Efraimu, Yuda lazima alime, naye Yakobo lazima avunjavunje mabonge ya udongo.
12 Sowe to your selues in righteousnes: reape after the measure of mercy: breake vp your fallowe grounde: for it is time to seeke the Lord, till he come and raine righteousnesse vpon you.
Jipandieni wenyewe haki, vuneni matunda ya upendo usio na kikomo, vunjeni ardhi yenu isiyolimwa; kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuwanyeshea juu yenu haki.
13 But you haue plowed wickednesse: ye haue reaped iniquitie: you haue eaten the fruite of lies: because thou didest trust in thine owne waies, and in the multitude of thy strong men,
Lakini mmepanda uovu, mkavuna ubaya, mmekula tunda la udanganyifu. Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe na wingi wa mashujaa wenu,
14 Therefore shall a tumult arise among thy people, and all thy munitions shall be destroyed, as Shalman destroyed Beth-arbell in the daie of battell: the mother with the children was dashed in pieces.
mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.
15 So shall Beth-el doe vnto you, because of your malicious wickednes: in a morning shall the King of Israel be destroied.
Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.