< Exodus 23 >

1 “You must not spread stories that are lies. You must not help bad people by giving evidence that's malicious.
Haupaswi kutoa taarifa ya uongo kuhusu yeyote. usijiunge na mwanaume muovu kuwa shahidi wa uongo.
2 Don't follow the crowd in doing wrong. When you give evidence in a lawsuit, don't corrupt justice by siding with the majority.
Haupaswi kufuata umati kufanya uovu, wala kutoa ushahidi ukiwa na umati ili kupotosha haki.
3 Don't show favoritism to poor people in their legal cases either.
Haupaswi kumpendelea mwanaume maskini kwenye kesi yake.
4 If you come across your enemy's ox or donkey that has wandered off, take it back it to him.
Ukikutana na ng'ombe wa adui wako au punda wake amepotea, lazima umrudishie.
5 If you see the donkey of someone who hates you that has fallen under its load, don't just leave it there. You must stop and help.
Ukiona punda wa yule anaye kuchukia ameanguka chini na mzigo wake, hauta muacha huyo mtu. Lazima umsaidie na punda wake
6 You must not prevent the poor from getting justice in their lawsuits.
Haupaswi kupotosha haki kama yapaswa kwenda kwa watu maskini katika kesi ya mwanaume maskini.
7 Don't have anything to do with making false accusations. Don't kill the innocent or those who do right, for I won't let the guilty go unpunished.
Usijiunge na wengine kufanya shutuma za uongo, na usiue asiye na hatia wala mwenye haki, kwa kuwa sitamuacha muovu.
8 Don't accept bribes, for a bribe blinds those who can see, and undermines the evidence of the honest.
Husiwai chukuwa rushwa, kwa kuwa rushwa inawapofusha wanaoona, na kupotosha maneno ya wakweli.
9 Don't abuse foreigners living among you, since you know very well what it's like to be foreigners, for you were once foreigners in Egypt.
Haupaswi kumnyanyasa mgeni, kwa kuwa wewe ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri.
10 Six years you are to sow your land and harvest crops,
Kwa miaka sita utapanda mbegu kwenye nchi yako na kukusanya mazao yake.
11 but in the seventh year you are to let it rest and leave it uncultivated, so that poor people may eat what grows naturally from the field and the wild animals can finish what's left. Follow the same procedure for your vineyards and olive groves.
Lakini katika mwezi wa saba utaacha hakujalimwa, ili kwamba maskini miongoni mwenu wale. Wanacho acha, wanyama wa porini watakula. Utafanya hivyo na mashamba yenu ya mizabibu na ya mizaituni.
12 You have six days to do your work, but on the seventh day you must stop working, so that your ox and your donkey can rest, and your slaves' families can catch their breath, as well as the foreigners living among you.
Wakati wa siku sita utafanya kazi, lakini siku ta saba utapumzika. Fanya hivi ili ng'ombe na punda wako wapumzike, na ili wana wa watumwa wako wa kike na wageni wapumzike na kupata hauweni.
13 Make sure to pay attention to everything I've told you. Don't think to call on the names of other gods—you must not even mention them.
Kuwa makini kwa kila kitu nilicho kwambia. Husitaje majina ya miungu mingine, wala kuruhusu majina yao kusikika kutoka mdomoni mwako.
14 Three times every year you are to celebrate a feast dedicated to me.
Lazima usafiri kusherehekea mara tatu kwa ajili yangu kila mwaka.
15 You are to observe the Festival of Unleavened Bread as I instructed you. You are to eat bread without yeast for seven days at the appropriate time in the month of Abib, because that was the month you left Egypt. No one can come before me without bringing an offering.
Lazima uadhimishe sherehe ya Mkate usiotiwa Chachu. Kama nilivyo kuamuru, utakula mkate usiotiwa chachu kwa siku saba. Wakati huo, utajitokeza kwangu mwezi wa Abibu, uliowekwa kwa ajili ya kusudi hili. Ni kwa mwezi huu uliyo toka Misri. Lakini usijitokeze kwangu mikono mitupu.
16 You are also to observe the Festival of Harvest when you present the firstfruits of the produce from what you've sown in the fields. Lastly you are to observe the Festival of Gathering-In the Harvest at the end of the year, when you gather in the harvest of the rest of your crops from the field.
Lazima uadhimishe Sherehe ya Mavuno, matunda ya kwanza ya kazi yako ulipo panda mbegu shambani. Pia lazima uadhimishe Sherehe ya Ukusanyaji wa mwisho wa mwaka, unapo kusanya mazao yako kutoka shambani.
17 Every Israelite male is to come before the Lord God at these three times every year.
Wanaume wote wako lazima wajitokeze kwa Bwana Yahweh mara tatu kila mwaka.
18 You must not offer the blood of my sacrifices together with anything that contains yeast, and the fat from the offerings presented at my festival must not be left until morning.
Haupaswi kutoa damu iliyo tolewa dhabihu kwangu na mkate uliyotiwa hamira. Mafuta kutoka kwa dhabihu za sherehe zangu hayapaswi kubaki usiku wote mpaka asubui.
19 Bring the best firstfruits of your crops to the house of the Lord your God. Don't cook a young goat in its mother's milk.
Lazima ulete matunda ya kwanza bora kutoka shambani mwako ndani ya nyumba yangu, nyumba ya Yahweh Mungu wako. Haupaswi kumchemsha mbuzi mtoto akiwa bado ananyonya.
20 Look, I'm sending an angel ahead of you to protect you on the way and to take you to the place I've prepared for you.
Ninaenda kumleta malaika mbele yako kukuongoza njiani, na kukuleta sehemu niliyo iandaa.
21 Make sure you pay attention to him and do what he says. Don't oppose him, because he won't forgive rebellion, for he carries my authority.
Kuwa makini naye na kumtii.
22 However, if you listen to him carefully, and do everything that I tell you, then I will be an enemy to your enemies and I will fight those who fight against you.
Husimkasirishe, kwa kuwa hatasamehe makosa yako. Jina langu liko kwake. Kama hakika ukimtii sauti yake na kufanya kila ninacho kwambia, kisha nitakuwa adui kwa adui zako na mpinzani kwa wapinzani wako.
23 For my angel will go ahead of you and take you into the land of the Amorites, Hittites, Perizzites, Canaanites, Hivites, and Jebusites, and I will wipe them out.
Malaika mwangu ataenda mbele zako na kukuleta kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanani, Wahivi, na Wayebusi. Nitawaharibu.
24 You must not bow down to their gods or worship them or follow their pagan practices. No, you must demolish their idols and smash their sacred pillars into pieces.
Haupaswi kuinamia miungu yao, kuabudu, au kufanya wanavyo fanya. Badala yake, lazima uwapindue kabisa na kuvunja nguzo zao za mawe vipande vipande.
25 You are to worship the Lord your God, and he will bless your food and water. I will make sure none of you fall sick.
Lazima umuabudu Yahweh Mungu wako, na atabariki mkate wako na maji. Nitaondoa magonjwa miongoni mwenu.
26 No woman will have a miscarriage or be without children. I will make sure you live long lives.
Hakuna mwanamke atakaye kuwa tasa au mimba kuharibika katika nchi yako. Nitawapa maisha marefu.
27 I will send terror about me ahead of you which will throw every nation you meet into panic. I will make all your enemies turn and run away.
Nitatuma hofu yangu kwao ambao mnaenda. Nitaua wote mnao kutana nao. Nitafanya maadui zenu wawaogope kwa kugeuza migongo yao kwenu.
28 I will send hornets ahead of you to drive out before you the Hivites and Canaanites and Hittites.
Nitatuma mavu kwenu watakao fukuza Wahivi, Wakanani, na Wahiti mbele zenu.
29 I will not drive them out in just one year, because the land would become desolate and you would have to deal with increased numbers of wild animals.
Sitawaondoa kwenu kwa mwaka mmoja, au nchi itakuwa imetelekezwa, na wanyama wa porini watakuwa wengi kwenu.
30 Bit by bit I will drive them out ahead of you, until there are enough of you to take possession of the land.
Badala yake, nitawafukuza kidogo kidogo kutoka kwenu mpaka utakapo kuwa umestawi na kurithi nchi.
31 I will fix your borders from the Red Sea to the Sea of the Philistines, and from the desert to the Euphrates River. I will hand the inhabitants of the land over to you, and you will drive them out.
Nitatengeneza mipaka yako kutoka Bahari ya Shamu hadi Bahari ya Wafilisti, na kutoka nyikani hadi Mto Frati. Nitakupa ushindi juu ya wakazi wote wa nchi. Utawaondoa kutoka kwako mwenyewe.
32 You must not make any agreement with them or with their gods.
Haupaswi kufanya agano na wao au na miungu yao.
33 They must not be allowed to stay in your land, otherwise they will lead you to sin against me. For if you worship their gods, they will definitely become a trap for you.”
Hawapaswi kuishi nchini mwako, au watakufanya ufanya dhambi dhidi yangu. Ukiabudu miungu yao, hakika watakuwa mtego kwako.'”

< Exodus 23 >