< Dommer 20 >

1 Da droge alle Israels Børn ud, og Menigheden blev samlet som een Mand, fra Dan indtil Beersaba og Landet Gilead, til Herren i Mizpa.
Ndipo watu wote wa Israeli wakatoka kama mtu mmoja, toka Dani mpaka Beer-sheba, pamoja na nchi ya Gileadi; nao wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
2 Og Høvdingerne for hele Folket, alle Israels Stammer, stillede sig frem i Guds Folks Forsamling: Fire Hundrede Tusinde Mand Fodfolk, som kunde føre Sværd.
Viongozi wa watu wote, wa kabila zote za Israeli, wakachukua nafasi zao kwenye kusanyiko la watu wa Mungu-watu 400, 000 waendao kwa miguu, ambao walikuwa tayari kupigana na upanga.
3 Og Benjamins Børn hørte, at Israels Børn vare dragne op til Mizpa; og Israels Børn sagde: Siger, hvorledes er dette onde sket?
Basi wana wa Benyamini waliposikia kwamba watu wa Israeli walikuwa wamepanda Mispa. Wana wa Israeli wakasema, “Tuambieni ni kwa namna gani huu uovu umefanyika.”
4 Da svarede den levitiske Mand, Manden til den Kvinde, som var ihjelslagen, og sagde: Jeg og min Medhustru kom til Gibea, som hører Benjamin til, for at blive der om Natten.
Mlawi, mume wa mwanamke aliyeuawa, akajibu, Nilikuja Gibea katika nchi ya Benyamini, mimi na suria wangu, ili tulale.
5 Og Mændene i Gibea stode op imod mig og omringede mig i Huset om Natten; de tænkte at ihjelslaa mig, og de have krænket min Medhustru, saa at hun er død.
Wakati wa usiku, viongozi wa Gibea walinishambulia, wakizunguka nyumba na wakakusudia kuniua. Walimkamata na kumbaka suria wangu, naye akafa.
6 Da tog jeg fat paa min Medhustru og huggede hende i Stykker og sendte hende om til al Israels Arvs Land; thi de have gjort en Skændsel og en Daarlighed i Israel.
Nilimchukua suria wangu na kumkata mwili wake vipande vipande, na kuweka katika kila nchi ya urithi wa Israeli, kwa sababu wamefanya uovu huo na upumbavu katika Israeli.
7 Se, alle I ere Israels Børn; taler tilsammen og raadslaar her!
Sasa, ninyi Waisraeli wote, toeni maneno na ushauri wenu hapa.”
8 Da gjorde alt Folket sig rede som een Mand og sagde: Vi ville ikke, at nogen gaar til sit Telt, og at nogen viger herfra til sit Hus.
Watu wote wakaondoka pamoja kama mtu mmoja, wakasema, Hakuna hata mmoja wetu atakayeenda hemani kwake, wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
9 Men det er nu den Gerning, som vi ville gøre mod Gibea: Vi ville drage mod den efter Lodkastning.
Lakini sasa hivi ndivyo tutakavyoifanyia Gibea tutaishambulia kama kura inavyotuongoza.
10 Og vi ville tage ti Mænd af hundrede, af alle Israels Stammer, og hundrede af Tusinde, og tusinde af ti Tusinde, at de hente Tæring til Folket, at de kunne, naar de komme til Gibea i Benjamin, gengælde den al den Daarlighed, som den har gjort i Israel.
Tutachukua watu kumi katika mia moja katika makabila yote ya Israeli, na mia moja katika elfu, na elfu moja katika elfu kumi, kuwapa chakula kwa ajili ya watu hawa, ili waweze kufika Gibea katika Benyamini, watawaadhibu kwa uovu wao waliofanya katika Israeli.
11 Saa bleve alle Israels Mænd samlede mod Staden; som een Mand vare de forbundne.
Basi askari wote wa Israeli wakakusanyika juu ya mji, kama mtu mmoja.
12 Og Israels Stammer sendte Mænd til alle Benjamins Slægter og lode sige: Hvad er dette for en Ondskab, som er sket iblandt eder?
Makabila ya Israeli waliwatuma watu kwa kabila lote la Benyamini, wakisema, “Uovu huu uliofanywa kati yenu ni nini?
13 Saa giver nu de Mænd hid, de Belials Børn, som ere i Gibea, at vi kunne slaa dem ihjel og borttage det onde af Israel; men Benjamins Børn vilde ikke høre deres Brødres, Israels Børns, Bøst.
Kwa hiyo, tupeni watu hao waovu wa Gibea, tupate kuwaua, na hivyo tutaondoa kabisa uovu huu kutoka kwa Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakusikiliza sauti ya ndugu zao, watu wa Israeli,
14 Og Benjamins Børn bleve samlede fra Stæderne til Gibea, til at drage ud til Krigen mod Israels Børn.
Ndipo wana wa Benyamini wakakusanyika kutoka mijini kwenda Gibea, wakajiandaa kupigana na wana wa Israeli.
15 Og Benjamins Børn fra Stæderne bleve samme Dag talte, seks og tyve Tusinde Mand, som kunde føre Sværd, foruden Indbyggerne i Gibea, som bleve talte, syv Hundrede udvalgte Mænd.
Watu wa Benyamini wakakusanya kutoka miji yao ili kupigana siku ile, askari elfu ishirini na sita waliopangwa kupigana na upanga. Walakini, kuna watu mia saba waliochaguliwa kutoka kwa wenyeji wa Gibea.
16 Iblandt alt dette Folk vare syv Hundrede udvalgte Mænd, som vare kejthaandede, af hvilke enhver slyngede med en Sten paa et Haar og fejlede ikke.
Miongoni mwa askari wote hawa walikuwa watu mia saba waliochaguliwa ambao walikuwa wenye shoto. Kila mmoja wao angeweza kupiga unywele kwa mawe na asikose.
17 Men Mændene af Israel, foruden dem af Benjamin, bleve talte, fire Hundrede Tusinde Mand, som kunde føre Sværd; enhver af dem var Krigsmand.
Watu wa Israeli, bila kuhesabu namba kutoka kwa Benyamini, walikuwa na watu 400, 000 waliokuwa wamejifunza kupigana na upanga. Wote hawa walikuwa watu wa vita.
18 Da gjorde de sig rede og droge op til Guds Hus og adspurgte Gud, og Israels Børn sagde: Hvo skal drage op for os at begynde Krigen mod Benjamins Børn? og Herren sagde: Juda skal begynde.
Watu wa Israeli waliondoka, wakaenda Betheli, wakaomba ushauri kutoka kwa Mungu. Wakauliza, “Ni nani kwanza atakayewaangamiza watu wa Benyamini kwa ajili yetu?” Bwana akasema, “Yuda atashambulia kwanza.”
19 Saa gjorde Israels Børn sig rede om Morgenen, og de lejrede sig imod Gibea.
Watu wa Israeli waliamka asubuhi na wakahamisha kambi yao karibu na Gibea.
20 Og hver Mand af Israel gik ud til Krigen imod Benjamin, og hver Mand af Israel rustede sig til Krig mod dem, mod Gibea.
Watu wa Israeli walikwenda kupigana na Benyamini. Wakaweka nafasi zao za vita dhidi yao huko Gibea.
21 Da gik Benjamins Børn ud af Gibea, og de sloge af Israel paa den samme Dag to og tyve Tusinde Mand til Jorden.
Watu wa Benyamini wakatoka Gibea, nao wakawaua watu elfu ishirini na mbili wa jeshi la Israeli siku ile.
22 Men Folket af Israels Mænd styrkede sig og stillede sig atter op til Slag paa det samme Sted, hvor de havde stillet sig op paa den første Dag.
Wana wa Israeli walijitia nguvu wenyewe, na wakaunda mstari wa vita mahali pale walipokwisha kuchukua nafasi siku ya kwanza.
23 Og Israels Børn droge op og græd for Herrens Ansigt indtil Aften, og de adspurgte Herren og sagde: Skal jeg ydermere blive ved at drage op til Krig mod Benjamins, min Broders, Børn? og Herren sagde: Drager op mod ham!
Na wana wa Israeli wakaenda, wakalia mbele za Bwana hata jioni. Walitaka mwongozo kutoka kwa Bwana “Je, tunapaswa kwenda tena kupigana na ndugu zetu, watu wa Benyamini?” Naye Bwana akasema, “Wapigeni!”
24 Og Israels Børn kom nær til Benjamins Børn paa den anden Dag.
Basi watu wa Israeli wakapigana na askari wa Benyamini siku ya pili.
25 Og Benjamin gik ud fra Gibea imod dem paa den anden Dag, og de sloge af Israels Børn endnu atten Tusinde Mænd til Jorden; alle disse kunde føre Sværd.
Siku ya pili, Benyamini alitoka kupigana nao kutoka Gibea, nao wakawaua watu wa Israeli elfu kumi na nane. Wote walikuwa watu ambao walijifunza kupigana na upanga.
26 Da droge alle Israels Børn op, ja alt Folket, og kom til Guds Hus og græd og bleve der for Herrens Ansigt, og de fastede den samme Dag indtil Aften, og de ofrede Brændofre og Takofre for Herrens Ansigt.
Basi askari wote wa Israeli na watu wote wakaenda Betheli, wakalia, wakakaa mbele za Bwana; nao wakafunga siku hiyo hata jioni, wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
27 Og Israels Børn adspurgte Herren; og Guds Pagts Ark var der i de Dage.
Wana wa Israeli wakamwomba Bwana, - kwa sababu ya sanduku la agano la Mungu lilikuwapo siku hizo;
28 Og Pinehas, en Søn af Eleasar, Arons Søn, stod for hans Ansigt i de Dage og sagde: Skal jeg blive ved ydermere at drage ud til Krig imod Benjamins, min Broders, Børn, eller lade af? og Herren sagde: Drager op; thi i Morgen vil jeg give ham i din Haand.
na Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni, aliyekuwa akihudumia mbele ya sanduku siku hizo. “Je twende vitani tena dhidi ya watu wa Benyamini, ndugu zetu, au tuache?” Bwana akasema, “Wapigeni, kwa maana kesho nitawasaidia kuwashinda.
29 Og Israel satte Baghold ved Gibea trindt omkring.
Basi Israeli akaweka watu mahali pa siri karibu na Gibea.
30 Saa droge Israels Børn op imod Benjamins Børn paa den tredje Dag, og de stillede sig op imod Gibea, som to Gange tilforn.
Watu wa Israeli wakapigana na wana wa Benyamini kwa siku ya tatu, nao wakajenga vita vyao juu ya Gibea, kama walivyotangulia.
31 Da gik Benjamins Børn ud imod Folket, de droges bort fra Staden, og de begyndte at ihjelslaa nogle af Folket, som to Gange tilforn, paa de alfare Veje, af hvilke een løber op til Bethel og een til Gibea paa Marken, henved tredive Mand i Israel.
Watu wa Benyamini wakaenda kupigana na watu, nao wakachukuliwa mbali na mji. Walianza kuua baadhi ya watu. Kulikuwa na watu thelathini wa Israeli ambao walikufa katika mashamba na barabara. Njia moja ilienda Betheli, na nyingine ikaenda Gibea.
32 Da sagde Benjamins Børn: De ere slagne for vort Ansigt ligesom i Førstningen; men Israels Børn sagde: Lader os fly, at vi kunne drage ham bort fra Staden, paa de alfare Veje.
Ndipo wana wa Benyamini wakasema, “Wameshindwa na wanatukimbia, kama hapo awali.” Lakini askari wa Israeli wakasema, “Hebu tukimbie na kuwavuta mbali na mji hadi barabarani.”
33 Da gjorde alle Israels Mænd sig rede af deres Sted og stillede sig op i Baal-Thamar, og Israels Baghold drog ud fra deres Sted, fra Hulen ved Geba.
Watu wote wa Israeli waliondoka kutoka mahali pao na wakajipanga kwa vita huko Baal-Tamari. Basi askari wa Israeli waliokuwa wakijificha mahali pa siri walikimbia kutoka Maare-Geba.
34 Og ti Tusinde Mand, udvalgte af al Israel, kom tværs over for Gibea, og Krigen blev svar; men den vidste ikke, at det onde skulde ramme den.
Wakatoka juu ya Gibea watu kumi elfu waliochaguliwa kutoka Israeli yote, na vita vilikuwa kali, lakini Wabenjamini hawakujua kwamba msiba ulikuwa karibu nao.
35 Saa slog Herren Benjamin for Israels Ansigt, og Israels Børn sloge af Benjamin paa den samme Dag fem og tyve Tusinde og hundrede Mand; alle disse kunde føre Sværd.
Bwana akamshinda Benyamini mbele ya Israeli. Siku hiyo, askari wa Israeli waliwauawa watu wa Benyamini 25, 100. Wote hawa waliokufa walikuwa wale waliokuwa wamejifunza kupigana na upanga.
36 Og Benjamins Børn saa, at de vare slagne; thi Israels Børn gave Benjamin Rum, fordi de forlode sig paa Bagholdet, som de havde lagt mod Gibea.
Basi askari wa Benyamini waliona wameshindwa. Wana wa Israeli walikuwa wametoa ardhi kwa Benyamini, kwa kuwa walikuwa wakihesabu watu waliowaweka katika nafasi zilizofichwa nje ya Gibea.
37 Og Bagholdet skyndte sig og faldt ind paa Gibea; og Bagholdet drog frem og slog den ganske Stad med skarpe Sværd.
Ndipo watu waliokuwa wameficha wakainuka na haraka na wakamkimbia Gibea. Nao wakauawa kila mtu aliyeishi mjini kwa upanga wao.
38 Og Mændene af Israel havde gjort en bestemt Aftale med Bagholdet, at de skulde lade megen og høj Røg opgaa af Staden.
Ishara iliyopangwa kati ya askari wa Israeli na watu waliojificha kwa siri itakuwa wingu kubwa la moshi litatokea nje ya mji.
39 Da vendte Israels Mænd sig i Slaget, og Benjamin havde begyndt at ihjelslaa af Israels Mænd henved tredive Mand; thi de sagde: Visseligen han er slagen for vort Ansigt som i det første Slag.
Ishara ilipokuja askari wa Israeli wakageuka kutoka kwenye vita. Basi Benyamini wakaanza kushambulia na wakawaua watu wa Israeli thelathini, wakasema, “Hakika wanapigwa mbele yetu, kama katika vita vya kwanza.”
40 Da begyndte en høj Røg, en Støtte af Røg, at stige op af Staden, og Benjamin saa om bag sig, og se, den hele Stad gik op i Røg mod Himmelen.
Lakini wakati nguzo ya moshi ilipoanza kuinuka nje ya mji, Wabenjamini waligeuka na kuona moshi ukitanda mbinguni kutoka mji mzima.
41 Og Israels Børn vendte sig, men Benjamins Mænd forfærdedes; thi de saa, at ondt vilde ramme dem.
Ndipo watu wa Israeli wakawageuka. Wana wa Benyamini waliogopa, kwa sababu waliona kwamba maafa yaliwajia.
42 Og de vendte sig for Israels Mænds Ansigt ad Vejen til Ørken, men Kampen indhentede dem; og de fra Stæderne nedhuggede dem midt imellem sig.
Basi wakakimbia kutoka kwa wana wa Israeli, kuelekea njia ya jangwani. Lakini vita viliwapata. Askari wa Israeli walitoka mijini na wakawaua pale waliposimama.
43 De omringede Benjamin, de forfulgte ham; hvor han hvilede, lode de ham nedtrædes, indtil tværs over for Gibea mod Solens Opgang.
Waliwalzungukia wana wa Benjamini na wakawafuata. Nao wakawakanyaga huko Noha, wakawaua mpaka upande wa mashariki wa Gibea.
44 Og der faldt af Benjamin atten Tusinde Mand; alle disse vare stridbare Mænd.
Kutoka kabila la Benyamini, watu kumi na nane elfu walikufa, wote walikuwa wanaume waliojulikana katika vita.
45 Da vendte de sig og flyede mod Ørken, til Klippen Rimmon, og hine sloge her og der paa de alfare Veje fem Tusinde Mand og forfulgte dem indtil Gideom, og de sloge af dem to Tusinde Mand.
Wakageuka na kukimbia kuelekea jangwani hadi mwamba wa Rimoni. Waisraeli waliuawa zaidi ya elfu tano kati yao barabarani. Waliendelea kuwafuata, wakifuata kwa njia kuu kwenda Gidomu, na huko waliuawa elfu mbili zaidi.
46 Og alle de, som faldt af Benjamin, vare fem og tyve Tusinde Mand, som kunde føre Sværd, paa den Dag; alle disse vare stridbare Mænd.
Askari wote wa Benyamini walioshuka siku hiyo walikuwa watu ishirini na tano waliokuwa wamejifunza kupigana kwa upanga; wote walikuwa wanajulikana katika vita.
47 Og seks Hundrede Mænd vendte sig og flyede mod Ørken til Klippen Rimmon; og de bleve paa Klippen Rimmon fire Maaneder.
Lakini watu mia sita wakageuka na kukimbilia jangwani, kuelekea mwamba wa Rimoni. Wakakaa katika mwamba wa Rimoni kwa muda wa miezi minne.
48 Og Israels Mænd vendte tilbage til Benjamins Børn og sloge dem med skarpe Sværd, baade Folket af Stæderne og Kvæget, ja alt det, som fandtes; ogsaa alle Stæderne, som fandtes, satte de Ild paa.
Askari wa Israeli waliwarudia watu wa Benyamini na wakawashinda na kuwaua-mji mzima, ng'ombe, na kila kitu walichopata. Pia walichoma moto kila mji katika njia yao.

< Dommer 20 >