< 4 Mojžišova 1 >

1 Mluvil pak Hospodin k Mojžíšovi na poušti Sinai, v stánku úmluvy, prvního dne měsíce druhého, léta druhého po vyjití jejich z země Egyptské, řka:
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2 Sečtěte summu všeho množství synů Izraelských po čeledech jejich, a po domích otců jejich, vedlé počtu jmen každého pohlaví mužského po hlavách jejich,
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3 Od dvadcítiletých a výše všecky, kteříž by mohli jíti k boji v Izraeli, sečtěte je po houfích jejich, ty a Aron.
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4 A bude s vámi z každého pokolení jeden muž, kterýž by přední byl v domě otců svých.
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5 Tato pak jsou jména mužů, kteříž stanou s vámi: Z pokolení Rubenova Elisur, syn Sedeurův;
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6 Z Simeonova Salamiel, syn Surisaddai;
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7 Z Judova Názon, syn Aminadabův;
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 Z Izacharova Natanael, syn Suar;
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9 Z Zabulonova Eliab, syn Helonův;
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10 Z synů Jozefových, z pokolení Efraimova Elisama, syn Amiudův; z Manassesova Gamaliel, syn Fadasurův;
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11 Z Beniaminova Abidan, syn Gedeonův;
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12 Z pokolení Dan Ahiezer, syn Amisaddai;
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13 Z Asser Fegiel, syn Ochranův;
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14 Z pokolení Gád Eliazaf, syn Duelův;
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15 Z Neftalímova Ahira, syn Enanův.
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16 Ti jsou slovoutní z lidu, knížata pokolení otců svých, ti jako hlavy tisíců Izraelských budou.
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17 Vzal tedy Mojžíš a Aron muže ty, kteříž jmenováni byli,
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18 A shromáždili všecko množství prvního dne měsíce druhého, kteříž přiznávali se k rodům svým po čeledech svých, po domích otců svých, a vedlé počtu jmen, od dvadcítiletých a výše po osobách svých.
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19 Jakož byl přikázal Hospodin Mojžíšovi, tak sčetl je na poušti Sinai.
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20 I bylo synů Rubena prvorozeného Izraelova, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, a podlé počtu jmen, po hlavách jejich, všech pohlaví mužského, od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž mohli jíti k boji,
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
21 A načteno jich z pokolení Rubenova čtyřidceti šest tisíců a pět set.
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22 Z synů Simeonových, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, sečtených jeho vedlé počtu jmen, po hlavách jejich, všech pohlaví mužského od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž mohli jíti k boji,
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
23 Načteno jich z pokolení Simeonova padesáte devět tisíců a tři sta.
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24 Z synů Gádových, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, podlé počtu jmen, od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž mohli bojovati,
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
25 Načteno jich z pokolení Gádova čtyřidceti pět tisíců, šest set a padesát.
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26 Z synů Judových, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, vedlé počtu jmen, od dvadcíti let a výše, všech, kteříž mohli jíti k boji,
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
27 Načteno jich z pokolení Judova sedmdesáte čtyři tisíce a šest set.
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28 Z synů Izacharových, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, podlé počtu jmen, od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž mohli jíti k boji,
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
29 Načteno jich z pokolení Izacharova padesáte čtyři tisíce a čtyři sta.
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30 Z synů Zabulonových, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, podlé počtu jmen, od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž mohli jíti k boji,
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
31 Načteno jich z pokolení Zabulonova padesáte sedm tisíců a čtyři sta.
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32 Z synů Jozefových, a nejprv, synů Efraimových, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, podlé počtu jmen, od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž mohli jíti k boji,
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
33 Načteno jich z pokolení Efraimova čtyřidceti tisíc a pět set.
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34 Potom z synů Manassesových, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, vedlé počtu jmen, od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž vycházeli k boji,
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
35 Načteno jich z pokolení Manassesova třidceti dva tisíce a dvě stě.
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36 Z synů Beniaminových, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, vedlé počtu jmen, od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž mohli jíti do boje,
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
37 Načteno jich z pokolení Beniaminova třidceti pět tisíců a čtyři sta.
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38 Z synů Dan, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, vedlé počtu jmen, od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž vycházeli k boji,
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
39 Načteno jich z pokolení Dan šedesáte dva tisíce a sedm set.
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40 Z synů Asser, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, vedlé počtu jmen, od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž mohli jíti na vojnu,
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
41 Načteno jich z pokolení Asser čtyřidceti jeden tisíců a pět set.
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42 Z synů Neftalímových, rodiny jejich, po čeledech jejich, po domích otců jejich, vedlé počtu jmen, od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž mohli jíti k boji,
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
43 Načteno jich z pokolení Neftalímova padesáte tři tisíce a čtyři sta.
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44 Ten jest počet těch, kteréž sečtl Mojžíš a Aron a knížata Izraelská, dvanácte mužů, kteříž byli vybráni po jednom z domů otců svých.
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45 I bylo všech sečtených synů Izraelských po domích otců jejich, od dvadcítiletých a výše, všech, kteříž mohli vycházeti k boji v Izraeli,
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46 Všech sečtených bylo šestkrát sto tisíc, a tři tisíce, pět set a padesáte.
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47 Levítové pak vedlé pokolení otců svých nejsou počítáni mezi ně.
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48 Nebo byl mluvil Hospodin k Mojžíšovi, řka:
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49 Pokolení Levítského nebudeš počítati, a nepřičteš jich k synům Izraelským,
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50 Ale ustanovíš Levíty nad příbytkem svědectví, a nade vším nádobím jeho, a nade všemi věcmi, kteréž přináležejí k němu. Oni nositi budou příbytek i všecka nádobí jeho, oni přisluhovati budou jemu, a vůkol příbytku klásti se budou.
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51 Když se pak s místa bude míti hýbati příbytek, složí jej Levítové; a když se bude klásti příbytek, vyzdvihnou jej Levítové. Kdož by koli cizí přistoupil, umře.
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52 I budouť se klásti synové Izraelští, jeden každý v ležení svém, a jeden každý pod praporcem svým, a po houfích svých.
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53 Levítové pak klásti se budou vůkol příbytku svědectví, aby nepřišlo rozhněvání mé na shromáždění synů Izraelských; i budou Levítové držeti stráž u příbytku svědectví.
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54 Učinili tedy to synové Izraelští; všecko, jakž přikázal Hospodin Mojžíšovi, tak učinili.
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

< 4 Mojžišova 1 >