< Nehemiáš 6 >

1 I stalo se, když uslyšel Sanballat a Tobiáš, a Gesem Arabský i jiní nepřátelé naši, že bych vystavěl zed, a že nezůstalo v ní mezery, ačkoli jsem ještě až do toho času nevstavil vrat do bran,
Habari zilipofika kwa Sanbalati, Tobia, Geshemu Mwarabu, na adui zetu wengine kwamba nimejenga tena ukuta na hakuna nafasi iliyobakia ndani mwake, ingawa mpaka wakati huo sikuwa nimeweka milango kwenye malango,
2 Že poslal Sanballat a Gesem ke mně, řka: Přiď, a rozmluvíme spolu ve vsi na rovinách Ono. Ale oni mé zlé obmýšleli.
Sanbalati na Geshemu wakanitumia ujumbe huu: “Njoo, tukutane katika mojawapo ya vijiji katika nchi tambarare ya Ono.” Lakini walikuwa wakikusudia kunidhuru.
3 Takž jsem poslal k nim posly, řka: Dílo veliké dělám, protož nemohu odjíti. Což se má meškati dílo, když bych je opustě, k vám sjíti měl?
Kwa hiyo niliwatuma wajumbe kwao na majibu haya: “Kazi ninayoifanya ni kubwa sana, siwezi kuja. Kwa nini niiache kazi isimame nije kwenu?”
4 I posílali ke mně na týž způsob čtyřikrát, a odpověděl jsem jim týmiž slovy.
Mara nne walinitumia ujumbe wa namna iyo hiyo, na kila mara niliwapa jibu lile lile.
5 Potom poslal ke mně Sanballat na tentýž způsob po páté služebníka svého s listem otevřeným.
Basi, mara ya tano, Sanbalati akamtuma msaidizi wake kwangu akiwa na ujumbe wa aina ile ile, naye alikuwa amechukua mkononi mwake barua isiyofungwa,
6 V kterémž bylo psáno: Slyší se mezi národy, jakž Gasmu praví, že ty a Židé myslíte se zprotiviti, a že ty proto stavíš zed, abys králem jejich byl, jakž se to dokoná.
iliyokuwa imeandikwa: “Habari imeenezwa miongoni mwa mataifa, naye Geshemu anasema kwamba ni kweli, kuwa wewe na Wayahudi mnafanya hila ya kuasi, ndiyo sababu mnajenga ukuta. Zaidi ya hayo, kufuatana na taarifa hizi, karibuni utakuwa mfalme wao,
7 Také žes i proroky postavil, aby hlásali o tobě v Jeruzalémě, řkouce: Král v Judstvu. Nyní tedy uslyší král ty věci. Protož přiď, a poradíme se spolu.
na hata umewateua manabii wafanye tangazo hili kukuhusu wewe huko Yerusalemu: ‘Yuko mfalme katika Yuda!’ Sasa taarifa hii itarudishwa kwa mfalme. Basi njoo, tufanye shauri pamoja.”
8 Tedy poslal jsem k němu, řka: Neníť toho nic, což ty pravíš, ale sám sobě to vymýšlíš.
Nilimpelekea jibu hili: “Hakuna jambo kama hilo unalosema linalofanyika. Unalitunga tu kwenye kichwa chako.”
9 Nebo všickni ti nás ustrašiti se snažovali, myslíce: Oslábnou ruce jejich při díle, a nedokoná se to. Ale však ty, ó Bože, posilň rukou mých.
Wote walikuwa wakijaribu kutuogopesha, wakifikiri hivi: “Mikono ya watu italegea kiasi kwamba hawataweza kufanya kazi, nayo haitakamilika.” Lakini niliomba, “Ee Mungu, sasa nitie mikono yangu nguvu.”
10 A když jsem všel do domu Semaiáše syna Delaiášova, syna Mehetabelova, kterýž se byl zavřel, řekl mi: Sejděme se do domu Božího, do vnitřku chrámu, a zavřeme dvéře chrámové; nebo přijdou, chtíc tě zamordovati. A to v noci přijdou, aby tě zamordovali.
Siku moja nilikwenda nyumbani kwa Shemaya mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, ambaye alikuwa amefungwa ndani ya nyumba yake. Akasema, “Tukutane katika nyumba ya Mungu, ndani ya Hekalu, na tufunge milango ya Hekalu, kwa sababu watu wanakuja kukuua. Naam, wanakuja usiku kukuua.”
11 Jemuž jsem řekl: Takový-liž by muž, jako jsem já, utíkati měl? Aneb kdo jest tak, jako jsem já, ješto by vejda do chrámu, živ byl? Nevejduť.
Lakini nikasema, “Je, mtu kama mimi akimbie? Au mtu kama mimi aende Hekaluni kuokoa maisha yake? Sitakwenda!”
12 I poznal jsem, a aj, Bůh neposlal ho, ale proroctví to mluvil proti mně, že ho Tobiáš a Sanballat byli ze mzdy najali.
Nilitambua kwamba Mungu hakumtuma, bali alitabiri dhidi yangu kwa sababu Tobia na Sanbalati walikuwa wamemwajiri.
13 Proto pak ze mzdy byl najat, abych já ustrašen jsa, učinil to a zhřešil, aby mi to bylo u nich k zlé pověsti, čímž by mi utrhali.
Alikuwa ameajiriwa kunitisha ili kwa kufanya jambo hili nitende dhambi, kisha waweze kuniharibia jina langu na kuniaibisha.
14 Budiž pamětliv, můj Bože, na Tobiáše a Sanballata, podlé těch skutků jejich, i na Noadii prorokyni, a na jiné proroky, kteříž strašili mne.
Ee Mungu wangu, wakumbuke Tobia na Sanbalati kwa sababu ya yale waliyotenda. Pia kumbuka nabii mke Noadia na manabii wengine ambao wamekuwa wakijaribu kunitisha.
15 A tak dodělána jest zed ta pětmecítmého dne měsíce Elul v padesáti a dvou dnech.
Basi ukuta ukakamilika siku ya ishirini na tano mwezi wa Eluli, kazi ambayo ilichukua siku hamsini na mbili.
16 To když uslyšeli všickni nepřátelé naši, a viděli všickni národové, kteříž byli vůkol nás, ulekli se velmi; nebo poznali, že od Boha našeho působeno bylo dílo to.
Adui zetu wote waliposikia kuhusu hili, mataifa yote yaliyotuzunguka yakaogopa na kupoteza ujasiri, kwa sababu yalitambua kuwa kazi hii imefanyika kwa msaada wa Mungu wetu.
17 Také v těch dnech i listy často posílali přednější Judští k Tobiášovi, tolikéž od Tobiáše docházely k nim.
Pia katika siku hizo wakuu wa Yuda walikuwa wakituma barua nyingi kwa Tobia, nayo majibu yaliyotoka kwa Tobia yaliendelea kuwajia.
18 Nebo mnozí v Judstvu měli s ním přísahu, proto že byl zetěm Sechaniáše syna Arachova, a Jochanan syn jeho pojal byl dceru Mesullama syna Berechiášova.
Kwa kuwa watu wengi katika Yuda walikuwa wamemwapia Tobia, kwani alikuwa mkwewe Shekania mwana wa Ara, na Yehohanani mwanawe alikuwa amemwoa binti wa Meshulamu mwana wa Berekia.
19 K tomu i dobré činy jeho vypravovali přede mnou, a řeči mé vynášeli k němu. Listy pak posílal Tobiáš, aby mne ustrašil.
Zaidi ya hayo, walikuwa wakiniarifu jinsi Tobia alivyo mtu mwema, nao walimwambia kila kitu nilichosema. Naye Tobia alituma barua za kunitisha.

< Nehemiáš 6 >