< Psalmi 84 >

1 Zborovođi. Po napjevu “Tijesci”. Sinova Korahovih. Kako su mili stanovi tvoji, Jahve nad Vojskama!
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
2 Duša mi gine i čezne za dvorima Jahvinim. Srce moje i moje tijelo kliču Bogu živomu.
Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
3 I vrabac sebi log nalazi, i lastavica gnjezdašce gdje će položiti mlade svoje:
Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
4 a ja žrtvenike tvoje, Jahve nad Vojskama, Kralju moj i Bože moj! Blaženi koji prebivaju u Domu tvome slaveć' te bez prestanka!
Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
5 Blažen komu je pomoć u tebi dok se sprema na svete putove!
Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
6 Prolaze li suhom dolinom, u izvor je vode promeću i prva je kiša u blagoslov odijeva.
Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
7 Snaga im raste od časa do časa: dok ne ugledaju Boga na Sionu.
Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
8 Jahve, Bože nad Vojskama, čuj molitvu moju, poslušaj, Bože Jakovljev!
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
9 Pogledaj, štite naš, Bože, pogledaj lice pomazanika svoga!
Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
10 Zaista, jedan je dan u dvorima tvojim bolji od tisuću drugih. Volim biti na pragu Doma Boga svoga nego boraviti u šatorima grešnika.
Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
11 Jahve, Bog, sunce je i štit: on daje milost i slavu. Ne uskraćuje Jahve dobara onima koji idu u nedužnosti.
Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
12 Jahve nad Vojskama, blago onom tko se u te uzda.
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.

< Psalmi 84 >