< Mudre Izreke 17 >
1 Bolji je zalogaj suha kruha s mirom nego sa svađom kuća puna žrtvene pečenke.
Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
2 Razuman sluga vlada nad sinom sramotnim i s braćom će dijeliti baštinu.
Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
3 Taljika je za srebro i peć za zlato, a srca iskušava Jahve sam.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
4 Zločinac rado sluša usne prijevarne, i lažac spremno prisluškuje pogubnu jeziku.
Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
5 Tko se ruga siromahu, podruguje se Stvoritelju njegovu, i tko se veseli nesreći, ne ostaje bez kazne.
Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
6 Unuci su vijenac starcima, a sinovima ures oci njihovi.
Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
7 Ne dolikuje budali uzvišena besjeda, a još manje odličniku usne lažljive.
Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
8 Dar je čarobni kamen u očima onoga koji ga daje: kamo se god okrene, uspijeva.
Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
9 Tko prikriva prijestup, traži ljubav, a tko glasinu širi, razgoni prijatelje.
Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
10 Razumna se ukor jače doima nego bezumna stotina udaraca.
Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
11 Opak čovjek ide samo za zlom, ali se okrutan glasnik šalje na nj.
Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
12 Bolje je nabasati na medvjedicu kojoj ugrabiše mlade nego na bezumnika u njegovoj ludosti.
Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
13 Tko dobro zlom uzvraća neće ukloniti nesreću od doma svojeg.
Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
14 Zametnuti svađu isto je kao pustiti poplavu: stoga prije nego svađa izbije, udalji se!
Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
15 Tko opravdava krivoga i tko osuđuje pravoga, obojica su mrski Jahvi.
Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
16 Čemu novac u ruci bezumnomu? Da njime mudrost kupi, kad nema razbora!
Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
17 Prijatelj ljubi u svako vrijeme, a u nevolji i bratom postaje.
Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
18 Nerazuman čovjek daje ruku i jamči pred svojim bližnjim.
Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
19 Grijeh ljubi tko ljubi svađu, i tko visoko diže svoja vrata, traži propast.
Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
20 Opak srcem ne nalazi sreće, i komu je jezik zao, zapada u nesreću.
Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
21 Tko rodi bezumna, na tugu mu je; a nije veseo ni otac budale.
Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
22 Veselo je srce izvrstan lijek, a neveseo duh suši kosti.
Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
23 Opaki prima dar iz njedara da bi iskrivio putove pravici.
Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
24 Razuman ima mudrost pred sobom, a bezumniku su oči na kraj zemlje.
Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
25 Briga je ocu bezuman sin i žalost roditeljki svojoj.
Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
26 Ne valja kažnjavati pravednika, a nije pravo ni tući odličnike.
Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
27 Tko usteže svoje riječi, razumije mudrost, i razuman je čovjek mirna duha.
Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
28 I luđak se smatra mudrim kada šuti i razumnim kad susteže svoje usne.
Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.