< Brojevi 35 >

1 Reče Jahve Mojsiju na Moapskim poljanama kod Jordana, nasuprot Jerihonu:
Bwana akamwambia Mose katika nchi tambarare ya Moabu, kando ya Mto Yordani kuvukia Yeriko,
2 “Naredi Izraelcima da ustupe levitima od baštine koju posjeduju gradove gdje će stanovati i pašnjake oko gradova. To dajte levitima.
“Waagize Waisraeli kuwapa Walawi miji ya kuishi kutoka urithi ambao Waisraeli wataumiliki. Wape maeneo ya malisho kuzunguka hiyo miji.
3 Neka gradovi budu njima za stanovanje, a okolni pašnjaci neka budu za njihova goveda, njihovo blago i sve njihove životinje.
Kisha watakuwa na miji ya kuishi na maeneo ya malisho kwa ajili ya ngʼombe zao, mbuzi, kondoo na mifugo yao mingine yote.
4 Pašnjaci uz gradove koje ustupite levitima neka zahvate od gradskih zidina van do tisuću lakata naokolo.
“Maeneo ya malisho kuzunguka miji hiyo ambayo mtawapa Walawi yataenea mita 450 kutoka kwenye ukuta wa miji.
5 Izmjerite od grada van dvije tisuće lakata s istočne strane, dvije tisuće lakata s južne strane, dvije tisuće lakata sa zapadne strane i sa sjeverne strane dvije tisuće lakata, tako da grad bude u sredini. To neka im budu gradski pašnjaci.
Nje ya mji, pima mita 900 upande wa mashariki, upande wa kusini mita 900, upande wa magharibi mita 900, na upande wa kaskazini mita 900, na mji utakuwa katikati. Eneo hili litakuwa lao kwa ajili ya malisho.
6 Od gradova koje budete dali levitima šest će ih biti gradovi-utočišta, koje ćete ustupiti da ubojica može tamo pobjeći. Ovima dodajte još četrdeset i dva grada.
“Miji sita mtakayowapa Walawi itakuwa ya makimbilio, ambayo mtu anayemuua mwenzake aweza kukimbilia humo. Zaidi ya hiyo, wapeni miji mingine arobaini na miwili.
7 Tako će svih gradova koje ustupite levitima biti četrdeset i osam gradova s njihovim pašnjacima.
Kwa jumla inawapasa kuwapa Walawi miji arobaini na minane, pamoja na maeneo ya malisho yao.
8 A gradove koje budete izdvajali od vlasništva Izraelaca, od onih koji ih imaju mnogo uzmite više, a manje od onih koji imaju malo. Neka svatko ustupi gradove levitima prema omjeru baštine koju bude primio.”
Miji ambayo mtawapa Walawi kutoka nchi ambayo Waisraeli wanamiliki itatolewa kwa uwiano wa urithi wa kila kabila. Chukua miji mingi kutoka lile kabila lenye miji mingi, lakini uchukue miji michache kutoka kwa kabila lile lenye miji michache.”
9 Nadalje reče Jahve Mojsiju:
Kisha Bwana akamwambia Mose:
10 “Govori Izraelcima i reci im: 'Kad prijeđete preko Jordana u zemlju kanaansku,
“Sema na Waisraeli, uwaambie: ‘Mtakapovuka Yordani kuingia Kanaani,
11 označite sebi gradove koji će vam služiti kao gradovi-utočišta, kamo može pobjeći ubojica koji nehotice koga ubije.
chagueni baadhi ya miji iwe miji yenu ya makimbilio, ambayo mtu ambaye ameua mwenzake bila kukusudia aweza kukimbilia humo.
12 Ti gradovi neka vam budu utočište od osvetnika, tako da ubojica ne moradne poginuti dok ne stane na sud pred zajednicu.
Itakuwa mahali pa kukimbilia kutoka mlipiza kisasi, ili kwamba mtu aliyeshtakiwa kwa mauaji asife kabla ya kujitetea mbele ya mkutano.
13 Od gradova koje ustupite bit će vam šest gradova za utočište.
Miji hii sita mtakayoitoa itakuwa miji yenu ya makimbilio.
14 Dodijelite tri grada s onu stranu Jordana, a tri grada u zemlji kanaanskoj. Neka to budu gradovi-utočišta.
Mtatoa miji mitatu ngʼambo hii ya Yordani na miji mingine mitatu upande wa Kanaani kama miji ya makimbilio.
15 Tih šest gradova neka budu za utočište kako Izraelcima tako i strancu i došljaku koji među njima borave, kamo može pobjeći tko god ubije koga nehotice.
Miji hii sita itakuwa mahali pa makimbilio kwa ajili ya Waisraeli, wageni na watu wengine wanaoishi katikati yenu, ili kwamba mtu yeyote ambaye ameua mtu mwingine pasipo kukusudia aweze kukimbilia humo.
16 Ali ako tko udari koga gvozdenim predmetom te ga usmrti, to je onda ubojica. Ubojica mora glavom platiti.
“‘Kama mtu akimpiga mwenzake kwa chuma naye mtu huyo akafa, mtu huyo ni muuaji; muuaji sharti atauawa.
17 Udari li ga iz ruke kamenom od kojega čovjek može poginuti i zbilja pogine, to je opet ubojica. Ubojica mora glavom platiti.
Au kama mtu analo jiwe mkononi mwake ambalo laweza kuua, naye akampiga mwenzake akafa, yeye ni muuaji; muuaji huyo sharti atauawa.
18 Ili ako ga udari iz ruke kakvim drvenim predmetom od kojega može umrijeti i zbilja umre, i to je ubojica. Ubojica mora glavom platiti.
Au kama mtu ana chombo cha mti mkononi mwake ambacho chaweza kuua, naye akampiga mwenzake akafa, yeye ni muuaji; muuaji huyo sharti atauawa.
19 Krvni osvetnik mora sam ubojicu usmrtiti. Kad ga sretne, neka ga ubije.
Mlipiza kisasi cha damu atamuua muuaji; wakati akikutana naye, atamuua.
20 Nadalje, ako tko koga gurne iz mržnje ili na nj nešto baci namjerno te ga usmrti,
Ikiwa mtu ana chuki ya siku nyingi na mwenzake akamsukuma au akamtupia kitu kwa kukusudia naye akafa,
21 ili ga udari rukom iz zlobe te udareni umre, napadač mora zaglaviti - on je ubojica. Krvni osvetnik neka ubojicu ubije čim ga sretne.
au ikiwa katika uadui akampiga ngumi naye akafa, mtu yule sharti atauawa; yeye ni muuaji. Mlipiza kisasi cha damu atamuua muuaji atakapokutana naye.
22 No gurne li ga slučajno, ne iz neprijateljstva, ili nešto na nj baci, ali ne iz zasjede,
“‘Lakini kama mtu akimsukuma mwenziwe ghafula pasipo chuki, au kumtupia kitu pasipo kukusudia,
23 ili iz nepažnje na njega obori kakav kamen od kojega čovjek može poginuti te ga usmrti, a nije mu bio neprijatelj niti mu je zlo želio -
au, pasipo kumwona, akimwangushia jiwe ambalo laweza kumuua naye akafa, basi kwa kuwa hakuwa adui yake naye hakukusudia kumuumiza,
24 tada neka zajednica prosudi između ubojice i krvnog osvetnika prema ovim pravilima:
kusanyiko lazima liamue kati yake na mlipiza kisasi wa damu kufuatana na sheria hizi.
25 Zajednica mora izbaviti ubojicu iz ruku krvnog osvetnika; onda neka ga zajednica vrati u grad-utočište kamo je pobjegao; tu neka on ostane do smrti velikoga svećenika koji je bio pomazan svetim uljem.
Kusanyiko ni lazima limlinde yule anayeshtakiwa kuua kutoka kwa mlipiza kisasi wa damu, na kumrudisha katika mji wa makimbilio alikokuwa amekimbilia. Lazima akae humo mpaka atakapokufa kuhani mkuu ambaye alikuwa amepakwa mafuta matakatifu.
26 Ali ako ubojica ikad izađe izvan granice utočišta kamo je pobjegao,
“‘Lakini kama mshtakiwa atatoka nje ya mipaka ya mji wa makimbilio ambao amekimbilia,
27 pa na nj nabasa krvni osvetnik izvan granica njegova grada-utočišta te krvni osvetnik ubije ubojicu, to mu se ne računa u krvoproliće,
na mlipiza kisasi wa damu akamkuta nje ya mji, mlipiza kisasi wa damu anaweza kumuua mshtakiwa huyo bila kuwa na hatia ya kuua.
28 jer ubojica mora ostati u gradu-utočištu do smrti velikoga svećenika. A poslije smrti velikoga svećenika može se vratiti na svoj posjed.
Mshtakiwa lazima akae katika mji wake wa makimbilio mpaka atakapokufa kuhani mkuu; atarudi tu kwenye mali yake baada ya kifo cha kuhani mkuu.
29 Neka vam takvi budu sudbeni postupci od naraštaja do naraštaja svuda gdje budete boravili.
“‘Hizi ndizo kanuni za sheria zitakazohitajiwa kwenu na katika vizazi vyenu vijavyo, popote mtakapoishi.
30 Za svako ubojstvo čovjeka kazna smrti nad ubojicom može se izvršiti na dokaz svjedoka. Nitko se ne može smrću kazniti na dokaz samo jednog svjedoka.
“‘Yeyote anayeua mtu atauawa kama muuaji ikiwa tu kuna ushuhuda wa mashahidi. Lakini hakuna mtu atakayeuawa kwa ushuhuda wa shahidi mmoja tu.
31 Ne smijete primati otkupnine za život ubojice koji je zaslužio smrt: on mora umrijeti.
“‘Usikubali fidia yoyote ya kuokoa uhai wa muuaji ambaye anastahili kufa. Mtu huyo hakika lazima auawe.
32 Niti smijete primati otkupnine od bilo koga koji, pošto je pobjegao u svoj grad-utočište, hoće da se vrati i da živi na svome tlu prije smrti velikoga svećenika.
“‘Usikubali fidia ya mtu yeyote ambaye amekimbilia katika mji wa makimbilio na kumruhusu kurudi kuishi katika nchi yake kabla ya kifo cha kuhani mkuu.
33 Nemojte oskvrnjivati zemlje u kojoj živite. A krvoprolićem zemlja se oskvrnjuje. Za zemlju na kojoj je krv prolivena pomirenje se ne može pribaviti, osim krvlju onoga koji ju je prolio.
“‘Msiinajisi nchi mnayoishi. Umwagaji damu hunajisi nchi, na upatanisho hauwezekani kufanyika katika nchi ambayo damu imemwagwa, isipokuwa tu kwa damu ya yule aliyeimwaga damu.
34 Ne smije se obeščašćivati zemlja u kojoj živite i usred koje ja boravim, jer ja, Jahve, prebivam među sinovima Izraelovim.'”
Msiinajisi nchi mnayoishi, ambayo nami ninakaa, kwa kuwa Mimi, Bwana, ninakaa katikati ya Waisraeli.’”

< Brojevi 35 >