< 2 Ljetopisa 12 >

1 Kad je Roboam utvrdio kraljevstvo i ojačao, napustio je Jahvin zakon i on i sav Izrael s njim.
Baada ya nafasi ya Rehoboamu kuimarika na kuwa na nguvu, yeye na Israeli yote waliiacha sheria ya Bwana Mungu.
2 Ali pete godine Roboamova kraljevanja navali egipatski kralj Šišak na Jeruzalem, koji se bijaše iznevjerio Jahvi.
Kwa sababu hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu.
3 Došao je sa tisuću i dvjesta bojnih kola i sa šezdeset tisuća konjanika, a narodu koji je došao s njim iz Egipta - Libijcima, Sukijcima i Etiopljanima - nije bilo broja.
Akiwa na magari ya vita 1,200 na wapanda farasi 60,000 na idadi isiyohesabika ya majeshi ya Walibia, Wasukii na Wakushi yaliyokuja pamoja naye kutoka Misri.
4 Osvojivši tvrde judejske gradove, dopro je do Jeruzalema.
Akateka miji ya Yuda yenye ngome akaendelea mpaka Yerusalemu.
5 Tada dođe prorok Šemaja k Roboamu i judejskim knezovima, koji se bijahu skupili u Jeruzalemu bježeći od Šišaka, i reče im: “Ovako veli Jahve: 'Vi ste ostavili mene, pa i ja ostavljam vas u ruke Šišaku.'”
Ndipo nabii Shemaya akaja kwa Rehoboamu na kwa viongozi wa Yuda waliokuwa wamekusanyika huko Yerusalemu kwa ajili ya hofu ya Shishaki naye akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo, mimi nami sasa ninawaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.’”
6 Tada se poniziše izraelski knezovi i kralj i rekoše: “Pravedan je Jahve!”
Viongozi wa Israeli na mfalme wakajinyenyekeza na kusema, “Bwana Mungu ni mwenye haki.”
7 Kad ih Jahve vidje gdje se poniziše, dođe njegova riječ Šemaji: “Ponizili su se; neću ih uništiti, nego ću im uskoro dati spasenje te se moja srdžba neće oboriti na Jeruzalem preko Šišaka.
Bwana Mungu alipoona kwamba wamejinyenyekeza, neno hili la Bwana likamjia Shemaya: “Maadamu wamejinyenyekeza, sitawaangamiza bali hivi karibuni nitawapatia wokovu. Ghadhabu yangu haitamwagwa juu ya Yerusalemu kwa kupitia Shishaki.
8 Bit će mu sluge, da vide što znači služiti meni, a što zemaljskim kraljevstvima.”
Hata hivyo, watamtumikia Shishaki ili wapate kujifunza tofauti kati ya kunitumikia mimi na kuwatumikia wafalme wa nchi nyingine.”
9 Tako egipatski kralj Šišak navali na Jeruzalem, opljačka blago iz Doma Jahvina i riznicu kraljeva dvora; sve je uzeo; uze i zlatne štitove što ih bijaše napravio Salomon.
Shishaki mfalme wa Misri alipoishambulia Yerusalemu, alichukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
10 Namjesto njih kralj Roboam napravi tučane štitove i povjeri ih zapovjednicima straže koja je čuvala vrata kraljevskoga dvora.
Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
11 Kad je god kralj išao u Dom Jahvin, stražari su ih uzimali, a poslije ih vraćali u stražaru.
Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana walinzi walikwenda pamoja naye wakiwa wamebeba hizo ngao na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
12 Kad se, dakle, ponizio, odvratio se od njega Jahvin gnjev te ga nije sasvim uništio, jer i u Judeji bijaše dobra.
Kwa sababu Rehoboamu alijinyenyekeza, hasira ya Bwana ikageukia mbali naye, hakuangamizwa kabisa. Kukawa na hali nzuri katika Yuda.
13 Potom se kralj Roboam utvrdi u Jeruzalemu i stade kraljevati. Roboamu je bila četrdeset i jedna godina kad se zakraljio, a sedamnaest je godina kraljevao u Jeruzalemu, u gradu koji Jahve izabra između svih izraelskih plemena da ondje postavi Ime svoje. Majka mu se zvala Naama, a bila je Amonka.
Mfalme Rehoboamu akajiweka imara katika Yerusalemu na akaendelea kuwa mfalme. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na saba, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli ili aliweke Jina lake humo. Mama yake aliitwa Naama, alikuwa Mwamoni.
14 Činio je zlo, jer nije pregnuo srcem da traži Jahvu.
Rehoboamu akatenda maovu kwa sababu hakuuelekeza moyo wake katika kumtafuta Bwana Mungu.
15 Roboamova prva i posljednja djela - i ratovi koji su se neprestano vodili između Roboama i Jeroboama - zapisani su u povijesti proroka Šemaje i u plemenskom popisu vidioca Adona.
Kwa habari ya matukio katika utawala wa Rehoboamu, tangu mwanzo mpaka mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Shemaya na mwonaji Ido zinazohusiana na vizazi? Kulikuwako na vita mara kwa mara kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
16 Potom Roboam počinu sa svojim ocima i bi sahranjen u Davidovu gradu; na njegovo se mjesto zakraljio sin mu Abija.
Rehoboamu akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Ljetopisa 12 >